STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 8, 2015

Manchester Utd chupuchupu kufa ugenini

Falcao akijaribu kufunga
Kouyate akishangilia bao lake
Pilikapilika uwanjani
KLABU ya Manchester United imeponea chupu chupu kufa ugenini baada ya kupata sare ya 1-1 mbele yua West Ham United.

Bao la kusawazisha lililofungwa dakika za lala salama na Daley Blind liliwaokoa Mashetani Wekundu kufa katika uwanja wa Boleyn Ground.
Blind alifunga bao hilo katika dakika mbili za nyongeza na kumnusuru kocha Luis Van Gaal kuumbuka kama alivyonusurika kocha wa Manchester City jana dhidi ya Hull City baada ya vijana wake kusawazisha bao dakika za jioni.
Wenyeji walitangulia kupata bao dakika ya 49 kupitia kwa Cheikhou Kouyaté na kulikuwa na kila dalili kwa Mashetani Wekundu kufa ugenini, lakini Blind kuchomoa na kuifanya Manchester United kufikisha pointi 44 na kukomalia nafasi ya nne nyuma ya Southampton waliorejea katika Tatu Bora.
Hata hivyo dakika mbili za nyongeza baada ya Man kupata bao ilijikuta ikimpoteza beki wake, Luke Shaw kwa kupewa kadi nyekundu ilifuatia kutokana na kadi ya pili ya njano kwa kumchezea vibaya Stewart Downing.
Vikosi vilikuwa hivi; 
West Ham: Adrian, Jenkinson, Song, Tomkins, Cresswell, Kouyate, Noble, Downing, Nolan, Valencia, Sakho.
Sub: Jarvis, O'Brien, Amalfitano, Jaaskelainen, Cole, Oxford, Lee
Manchester United: De Gea, Valencia, Jones, Rojo, Shaw, Blind, Rooney, Januzaj, Di Maria, van Persie, Falcao
Sub: Mata, Smalling, Ander Herrera, Fellaini, Valdes, McNair, Wilson

No comments:

Post a Comment