STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 8, 2015

Asamoah Gyan bado alia na Yattara

http://img.modernghana.com/images/content/bgwi04lyx6_asamoahgyan580.jpg
Asamoah Gyan
NAHODHA wa kikosi cha timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan ambay anajiandaa kushuka dimbani kuiongoza timu yake katika mechi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Ivory Coast, amedai hatomsamehe golikipa wa Guinea Naby Yattara kutokana na faulo aliyomchezea timu zao zilipokutana.
Golikipa huyo alimkanyaga Gyan kwa teke la tumboni katika dakika za mwisho za mchezo wa robo fainali uliokutanisha timu hizo.
Yattara alilimwa kadi nyekundu lakini hajapewa adhabu yeyote nyingine mpaka sasa kiasi cha Gyan katika mahojiano yake alisema bado analitaka Shirikisho la Soka la Afrika(CAF) kumtwanga adhabu Yattara kwa sababu anadhani alidhamiria kufanya tukio lile.
Gyan aliendelea kudai kuwa ilikuwa ni faulo mbaya ambayo ingeweza kumsababisha asicheze tena soka ndio maana hataki kumsamehe kwa hilo.
Hata hivyo kipa huyo alinukuliwa juzi akisema kuwa hawezi kumuomba radhi Gyan kwa sababu hakukusudia kumuumiza na kusisitiza kuwa hilo ni tukio la bahati mbaya katika harakati za mchezo.

No comments:

Post a Comment