STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 8, 2015

Kocha Redknapp kurejea soka kama mwanahisa

http://talksport.com/sites/default/files/tscouk_old_image/blog/Harry-Redknapp_21.jpg
Kocha Harry Redknapp
MENEJA wa zamani wa klabu ya QPR, Harry Redknapp amebainisha anaweza kurejea katika ulimwengu wa soka akiwa sehemu ya mwanahisa.
Redknapp mwenye umri wa miaka 67 ambaye alijiuzulu kuinoa QPR wiki iliyopita kutokana na matatizo ya mguu anahusishwa na kikundi kinachotaka kununua klabu karibu na nyumbani kwake katka Pwani ya Dorset.
Akihojiwa Redknapp amesema jambo hilo linamvutia hivyo anataka kujihusha nalo, kwani mchezo wa soka bado uko katika damu yake.
Redknapp ambaye amewahi kuipeleka Tottenham Hotspurs katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na pia kuzinoa klabu za Portsmouth na West Ham United aliongeza kuwa wana matumaini ya kupata klabu ya kuinunua.

No comments:

Post a Comment