STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 8, 2015

Mchujo wa mabondia wa All African Games kuanza kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKf3j_9lbtaLQyaz_zQF0flGoPDNwRHy3gQ4ONfElr_vig3q8o4Qz8FPYmcPqZ0gMZDYrQgTaoGCdBXuRzDb3SOhXV60xTZTtAozbghUpubPSY0R6H4oYZPX0-B6AMkqUQhs2jWXY7oUw/s1600/antony.JPG
Mchujo kama huu unatarajiwa kuanza kesho Uwanja wa Ndani wa Taifa
http://www.thisday.co.tz/media/picture/large/BFTsecretary%20genera%20Makore%20Mashaga1.jpg
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga
MCHUJO wa kusaka mabondia wa kuingia kambini kwa ajili ya ushiriki wa michuano ya Michezo ya Afrika (All African Games) unatarajiwa kuanza kesho jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga alisema mashindano ya mchujo huo utafanyika kwenye Uwanja wa Ndani ya Taifa na utamalizika Siku ya Wapendanao Februari 14.
Mashaga alisema mashindano hayo maalum yatashirikisha walifanya vizuri katika mashindano ya wazi ya taifa yaliyofanyika hivi karibuni katika Uwanja wa Taifa.
"Mashindano maalum kwa ajili ya kusaka mabondia watakaotuwakilisha kwenye michezo ya Afrika yataanza Februari 9-14 Uwanja wa Ndani wa Taifa na utashirikisha waliofanye vema kwenye michuano ya wazi," alisema.
Kwa mujibu wa Mashanga mabondia 39 watachujana ili kupatikana 15 ili kuunda timu ya taifa ya mchezo huo wa ngumi.
Mashindano hao ya Mataifa ya Afrika yanatarajiwa kutimua vumbi lake kati ya Septemba 4-19 mjini Brazzaville, Congo na Tanzania ni miongoni mwa nchi shiriki.

No comments:

Post a Comment