STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 8, 2015

Jose Mourinho aanza mbwembwe zake England

http://static.guim.co.uk/sys-images/Observer/Columnist/Columnists/2013/6/7/1370621593808/jose-mourinho-010.jpg
Jose Mourinho
KOCHA wa vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea, Jose Mourinho amesema hadhani kama tofauti ya pointi saba walionayo kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo ni faida katika mbio zao za kugombea taji hilo. Chelsea imeitandika Aston Villa kwa mabao 2-1 jana, wakati Manchester City wanaowafuata katika nafasi ya pili wakipotoka sare na Hull City wanaokamata nafasi ya tatu toka mkiani.
Akihojiwa Kocha Mourinho, amesema ingekuwa nchi nyingine angeweza kuanza kushangilia katika kwa Uingereza tofauti ya alama saba sio chochote.
Mourinho aliendelea kudai kuwa bado kuna mechi 14 na alama 42 za kupigania hivyo kila mchezo unakuwa mgumu na chochote kinaweza kutokea.
Kocha huyo pia alisisitiza hakushtushwa kuona City wakitoa sare nyumbani na Hull ambao wako mstari wa kushuka daraja lakini amefurahi kuona matumaini ya kunyakuwa taji yakiwa mikononi mwao.
Ligi hiyo iliendelea tena jioni ya leo kwa timu za Newcastle United wakipata sare ya 1-1 na timu ya Stoke City wakati West Bromwich Albion wakiwa ugenini walipata sare ya 2-2 dhidi ya timu ya Burnley.

No comments:

Post a Comment