STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 14, 2013

Hizi ndizo mechi za VPL zinazosubiriwa kwa hamu Jumamosi

Kikosi cha Polisi Moro kinachopigana kuepuka kuteremka daraja

African Lyon iliyokwishashuka daraja
http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2012/09/139.jpg
Kikosi cha Toto kilichovitani kuepuka kurudi 'mchangani'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg97pj1ETW12r5ZB7z-OJ8AeGiP4rO7Ut270XLnChEjDivad0H0-rV1Af9HcJz2WAxYgIMJYzS-Rrrz-g_yDLcMerfoasb2tpWACsUj5YPZh7JzPT5nII4g5oYoBrntJnlrtmNWSdfen7Rz/s1600/Mgambo+JKT.jpg
Mgambo JKT nayo ipo kwenye mtego wa kurudi FDL

PAZIA la Ligi Kuu Tanzania bara linatarajiwa kufungwa rasmi siku ya Jumamosi kwa michezo saba tofauti, lakini ni mechi tatu tu kati ya hizo ndizo zitakazokuwa na mvuto na kufuatiliwa kwa karibu na mashabiki wa soka pengine kuliko hata pambano la watani wa jadi nchini, Simba na Yanga litakalochezwa Dar es Salaam.
Mechi hizo zitakazofuatiliwa kuliko la Simba na Yanga ambazo ni za kulinda heshima tu, ni ile ya jijini Mwanza kati ya wenyeji Toto Africans dhidi ya maafande wa Ruvu Shooting, itakayochezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
Hii ni kwa sababu Toto ipo katika janga la kushuka daraja na hivyo inahitaji ushindi huku ikiziombea Polisi Moro na Mgambo JKT ziteleze ili wenyewe waponee chupuchupu kama ilivyokuwa msimu uliopita.
Timu hiyo ina pointi 22 sawa na Polisi Moro na zinatofautiana idadi ya magoli ya kufunga na kufungwa na iwapo itashinda itafikisha pointi 25 ambazo tatari zimeshafikiwa na Mgambo JKT iyakayokushuka dimbani nyumbani jijini Tanga kuumana na Africans Lyon iliyokwisha kushuka daraja.
Polisi Moro ambayo ilizinduka kwenye duru la pili ilipochukuliwa na kocha Mohammed Rishard 'Adolph' kabla ya kuzorota tena yenyewe itakuwa nyumbani kuumana na Coastal Union.
Kwa kulinganisha mechi hizo tatu za wawania kuepuka kushuka daraja unaweza kuona angalau Mgambo ipo katika nafasi nzuri ya kuokoka kuliko Toto na Polisi, hii ni kwa sababu inamaliza mechi za msimu na Lyon iliyoshuka daraja kitambo, huku ikisaka pointi moja tu kuwaokoa, ingawa kwa mechi mbili mfululizo timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu imeshindwa kuipata mbele ya Simba na Azam.
Pazia la ligi hiyo mbali na mechi hizo na ile ya watani wa jadi, pia litafungwa na mechi nyingine tatu ambapo JKT Ruvu dhidi ya Mtibwa Sugar, Prisons na Kagera Sugar na lile la washindi wa pili na wawakilishi wa Kombe la Shirikisho kwa mara ya pili mwakani, Azam itakayokuwa ugenini mjini Arusha kuchuana na wenyeji wao JKT Oljoro.


                            P     W     D     L     F     A     D     Pts
Young Africans     25    17     6     2     45   14    31     57
Azam                    25   15     6     4     45    20   25     51   
Simba                   25    12    9     4     39     24  15     45
Kagera Sugar        25    11    8     6     27     20   7      41    
Mtibwa Sugar       25    10     9     6     29     24   5     39  
Coastal Union       25     8     11     6     25     22   3     35   
Ruvu Shooting       25     8     7     10     23     26  -3     31    
JKT Oljoro FC     25     7     8     10     22     28  -6     29    
Tanzania Prisons    25     7     8     10     16     22  -6     29   
Ruvu Stars            25     7     5     13     21     39   -18   26
JKT Mgambo       25     7     4     14     16     27   -11   25
Toto Africans        25     4     10    11     22     33  -11    22
Polisi Morogoro    25     4     10    11     13     23  -10    22   
African Lyon         25     5     4     16     16     38    -22   19
              

Mechi za kufungia pazia msimu wa 2012-2013

Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
Simba SC Vs Yanga SC
JKT Oljoro Vs Azam FC
Toto African Vs Ruvu Shooting
Polisi Moro Vs Coastal Union

TFF yafafanua kuhusu Ligi ya Mabingwa wa Mikoa


Na Boniface Wambura
LIGI ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) ilianza tarehe 12 Mei 2013 ikishirikisha klabu bingwa za mikoa yote ya Tanzania Bara, isipokuwa mikoa ya Pwani na Manyara ambayo kutokana na sababu tofauti ilishindwa kuwasilisha majina ya klabu zake hadi siku ya mwisho iliyowekwa na Kamati ya Mashindano, yaani tarehe 10 Mei 2013.

Suala la kukosekana kwa wawakilishi wa mikoa hiyo miwili limezua maswali mengi kiasi kwamba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linalazimika kutoa ufafanuzi kwa faida ya wadau wote wa mpira wa miguu.

Ligi ya Mabingwa wa Mikoa, ambayo ni mpya baada ya TFF kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa mpira wa miguu, ilipangwa kuanza tarehe 5 Mei 2013, lakini hadi tarehe ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, yaani tarehe 2 Mei 2013 mikoa michache ndiyo iliyokuwa imemaliza ligi zao na kupata mabingwa.

Kuchelewa huko kwa mikoa kumaliza ligi zao kuliilazimisha Kamati ya Mashindano ya TFF kuongeza muda wa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi hao hadi tarehe 10 Mei 2013 na hivyo siku ya kuanza kwa Ligi kusogezwa mbele hadi tarehe 12 Mei 2013.

Hadi kufikia tarehe hiyo mpya ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, ni mikoa sita tu iliyofaidika na kuongezwa huko kwa muda na kupata wawakilishi wake. Mikoa hiyo ni Iringa, ambayo pamoja na kuongezwa kwa muda, iliandika barua ya kuihakikishia Kamati ya Mashindano kuwa itapata bingwa kabla ya kuisha kwa siku ya tarehe 10 Mei 2013.

Mikoa mingine ni Lindi, Mtwara, Geita, Tabora na Dodoma.

Mkoa wa Manyara haukuweza kumaliza ligi yake hadi mwisho wa siku ya tarehe 10 Mei 2013 na hivyo Kamati ya Mashindano iliyosubiri majina hadi saa 12:00 jioni siku hiyo kuamua kuwaondoa wawakilishi wa Manyara kwenye ratiba.

Awali, Kamati ya Mashindano iliamua kuwa ratiba ya mechi za Ligi ya Mabingwa wa Mikoa ipangwe tarehe 7 Mei 2013, ikishirikisha mikoa ambayo ilishapata mabingwa wake, lakini baada ya kuona baadhi ya mikoa ilikuwa haijakamilisha ligi zake, Kamati iliamua kuwa ratiba ipangwe kwa kutumia majina ya mikoa kwa matumaini kuwa hadi kufikia tarehe 10 Mei 2013, mikoa itakuwa imeshapata wawakilishi wake na kwa kuwa ratiba inahusu mikoa jirani, ingekuwa rahisi kwa timu kusafiri kutoka kituo kimoja hadi kingine.

Lakini Mkoa wa Manyara haukuweza kufanya hivyo na Kamati kulazimika kuuondoa kwenye ratiba kutokana na kushindwa kukidhi utashi huo.

Mkoa mwingine ambao uliondolewa kwenye ratiba ni Pwani ambayo pamoja na kutuma jina la mwakilishi wake, Kamati ilipokea malalamiko kutoka klabu zilizoshiriki Ligi ya Mkoa, zikidai kuwa jina la bingwa wa Pwani lililowasilishwa TFF lilikuwa batili kwa kuwa klabu ya Kiluvia United haikustahili kushiriki Ligi ya Mkoa kutokana na ukweli kuwa haijasajiliwa mkoani Pwani na wala haikushiriki ligi ya mkoa msimu uliopita. Kamati ya Mashindano iliiondoa Pwani kwenye ratiba na kulirudisha suala hilo mkoani.

Ingawa Katibu wa Pwani alijaribu kuishawishi Sekretarieti ya TFF iliangalie suala hilo kwa undani zaidi, Sekretarieti ilimjibu kuwa lilishafanyiwa uamuzi na Kamati, hivyo uamuzi huo usingeweza kutenguliwa na kumshauri katibu huyo arejee mkoani kwake kuwasiliana na viongozi wenzake kuona ni jinsi gani mkoa unaweza kunusuru hali hiyo kwa kufanya uamuzi ambao ungeuwezesha mkoa kupata mwakilishi.

Kwa mantiki hiyo, masuala ya Manyara na Pwani yalikuwa ndani ya uongozi wa mikoa husika na si Kamati ya Mashindano ya TFF kwa kuwa Kamati ilitaka ipatiwe jina la bingwa ambaye alipatikana kwa mujibu wa mfumo mpya wa Ligi ya Mikoa.

Ligi ya Mabingwa wa Mikoa inachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na hivyo timu zilizokutana tarehe 12 Mei 2013, zitarudiana mwishoni mwa wiki hii na kupatikana timu zitakazosonga mbele kwenye raundi nyingine hadi timu tatu bora zitakazopanda daraja kwenda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zitakapopatikana.

Ligi za Mikoa, kwa mujibu wa kanuni mpya, zinatakiwa ziwe na timu kati ya 16 na 20 na zinatakiwa zicheze mechi mbili za nyumbani na ugenini, hata kama zitakuwa zinatumia uwanja mmoja.

Uamuzi wa kubadilisha mfumo huo ulifanywa ili kuhakikisha kuwa mikoa inakuwa na na mashindano kwa mwaka mzima na hivyo kuiwezesha mikoa kujikita katika kutafuta mbinu za kupata fedha na kuendeleza mchezo wa mpira wa miguu kwenye mikoa yao.

Uamuzi huo pia unasaidia kupunguza mtindo wa wachezaji kuzunguka klabu tofauti katika msimu mmoja kwa kuwa wanalazimika kutulia kwenye klabu moja hadi muda wa usajili unapofika.

Pamoja na wachezaji kutulia sehemu moja kwa muda mrefu, pia walimu wanapata fursa ya kujikita vizuri kwenye programu zao kwa kuwa wanakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya wachezaji wao.

Pamoja na hayo yote, mfumo huo utasaidia kurudisha msisimko kwenye mikoa na hivyo kutoa fursa kwa vijana wengi wenye vipaji kuonekana na kuendelezwa.

TFF inatoa wito kwa viongozi wa mikoa kuanza kubuni sasa mikakati ya kuendesha ligi hizo msimu unaokuja kwa kuwa hakutakuwa na nafasi tena ya kuongeza muda kwa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi wao.

Martin Saanya kuzihukumu Simba, Yanga viingilio vyatajwa


Vijana wa Yanga watacheka kama hivi Jumamosi?
Mwamuzi Martin Saanya atakayezihukumu Simba na Yanga

Vijana wa Simba nao watakenua kama hivi J'mosi Taifa?
Na Boniface Wambura
MWAMUZI Martin Saanya wa Morogoro ndiye aliyepewa jukumu la kuzihuku Simba na Yanga zitakazoumana siku ya Jumamosi kwenye pambano la kufungia msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara wa 2012-2013 litakalofanyika kwenye katika uwanja wa Taifa Dar es salaam.

Mwamuzi huyo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro, huku . Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.

Aidha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeanika viingilio vya pambano hilo la Jumamosi ambapo kiingilio cha chini kwenye mechi ya VPL kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.

Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.

Kocha Stars kuiteta Morocco kwa wanahabari

Kocha Kim Poulsen anayetarajiwa kuzungumza na wanahabari keshokutwa

Na Boniface Wambura
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya tiketi kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco. Mkutano huo utafanyika keshokutwa (Mei 16 mwaka huu) saa 5 kamili kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu kwenye jiji la Marrakech nchini Morocco. Taifa Stars ilishinda mechi yake iliyopita jijini Dar es Salaa kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Morocco.