STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 2, 2014

'Mjeda' awatungua risasi wawili na kuwaua mwaka mpya


MWANAJESHI wa Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ), ambaye jina lake limehifadhiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya  kuwaua kwa kuwapiga risasi vijana wawili na kisha kuwajeruhi vibaya wengine wawili walipokuwa katika shamrashamra za kuukaribisha mwaka mpya.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa sita na robo usiku wa kuamkia jana, katika eneo la Pugu Kinyamwezi, Ilala jijini Dar es Salaam.

Akizungumza  jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Marietha Minangi alisema tukio hilo lilitokea baada kundi la vijana waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya kuzingira gari la mwanajeshi huyo aliyekuwa akielekea nyumbani kwake Pugu Kinyamwezi, akitokea katikati ya Jiji kwa shughuli zake.

Alisema mwanajeshi huyo alikuwa na gari aina ya Toyota Rava 4 na  baada ya kufika katika eneo hilo alizingirwa  na  kundi la vijana hao waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya na ndipo aliamua kutoa  bastola yake na  kufyatua risasi ambapo iliwapata vijana hao na kufa papo hapo na kujeruhi wengine.

Aliwataja waliokufa katika tukio hilo kuwa ni Ibrahim Mohamed(16) mkazi wa Pugu Kinyamwezi, Abubakari Hassan(14) naye mkazi wa Pugu Kinyamwezi.

Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Rupano Wanga(17)  mkazi wa Pugu Makange na Kassim Abdul  (16), mwanafunzi wa shule ya sekondari Tandika.
Minangi alisema polisi walifanikiwa kumkamata mwanajeshi huyo na kumweka rumande  katika kituo cha polisi cha stakishari usiku huohuo.

Alisema vijana hao waliojeruhiwa walipelekwa Hospitali ya Amana kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.

Wakati huohuo, wakazi wa Kiwalani, Wilayani Temeke walipata wakati mgumu baada ya kutokea kwa kundi la vibaka waliokuwa wakipora simu, fedha na kutembeza mapanga kwa wakazi hao.

Kwa mujibu wa baadhi ya wakazi wa maeeno hayo, kundi hilo lilikuwa likizungukia kila nyumba na katika nyumba za starehe na kila aliyekutwa nje walichukua simu yake, fedha  na wengie kupigwa mapanga.

Yaya Toure 'anusa' tuzo nyingine Afrika


CAPE TOWN, Afrika Kusini
YAYA Toure anatarajiwa kutangazwa kuwa Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Afrika na kuifikia rekodi ya kuibeba tuzo hiyo mara tatu mfululizo baada ya kutajwa katika orodha ya wachezaji watatu walioingia fainali kwa ajili ya tuzo hiyo itakayotolewa mwezi huu.
Shirikisho la Soka Afrika (CAF) lilipunguza majina ya wanaoiwania tuzo hiyo 2013 kutoka 10, huku Toure akibaki na wachezaji 'wachovu' Didier Drogba (Ivory Coast) na John Obi Mikel (Nigeria/ Chelsea).
Jopo la makocha wa timu za taifa kutoka nchi 54 za Afrika litaamua mshindi, ambaye atatajwa katika hafla itakayofanyika mjini Lagos Januari 9.
Miongoni mwa waliokatwa katika orodha hiyo ni Mohamed Aboutrika, kiungo veterani wa Misri, ambaye Novemba aliiongoza klabu yake ya Al Ahli kutwaa taji la tano la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ndani ya miaka kumi iliyopita.
Mwingine aliyekatwa ni Jonathan Pitroipa, nyota wa timu ya taifa ya Burkina Faso ambayo iliukosa ubingwa wa Mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini mwanzoni mwa mwaka na kwenye kampeni za kufuzu kwa Kombe la Dunia.
Wote hao walitarajiwa kuwa washindani wa karibu zaidi wa Yaya Toure, ambaye anapewa nafasi kubwa kushinda kutokana na mafanikio binafsi katika mwaka ambao hapakuwa na wachezaji waliokuwa na mafanikio binafsi.
Toure aliisaidia Ivory Coast kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia na amerejea kuwa nguzo muhimu katika kikosi cha klabu yake ya Manchester City ya Ligi Kuu ya England.
Kama atafanikiwa kuitwaa tuzo hiyo, kiungo huyo atakuwa mchezaji wa tatu kuitwaa tuzo hiyo mara tatu mfululizo, akiwafikia Abedi Pele wa Ghana aliyeitwaa kuanzia 1991-93 na Samuel Eto'o kuanzia 2003 hadi 2005.
Mikel, ambaye anasota benchi katika klabu yake ya Chelsea, ametajwa kutokana na mchango wake katika kuisaidia Nigeria kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia na kutwaa ubingwa wa Mataifa ya Afrika mwanzoni mwa 2013.
Drogba ni mshindi mara mbili wa tuzo hiyo lakini straika huyo wa Galatasaray ameshangaza wengi kutajwa katika orodha ya walioingia fainali mwaka huu baada ya mwaka ambao alitemwa katika timu yake ya taifa ya Ivory Coast.

Manchester Man 'nyanya' kwa Tottenham

Adebayor akifuka juu kuupiga mpira uliozaa bao la kwanza la Spurs
Adebayor akiifungia Spurs bao la kuongoza
Oyoooooo! vijana wa Spurs wakishangilia bao lao la pili
MASHETANI Wekundu wamezidi kumweka pabaya kocha wake, David Moyes baada ya jana kupokea kipigo cha mabao 2-1 wakiwa nyumbani  mbele ya vijana wa Tottenham Hotspur.
Manchester Utd ambayo msimu huu imekuwa 'urojo' ilipokea kipigo hicho ikiwa ni mara ya kwanza baada ya kipindi kirefu kufungwa na Spurs nyumbani kwake.
Mabao ya Emmanuel Adebayor aliyefunga kipindi cha kwanza kwenye dakika ya 34 na jingine la Eriksen la dakika ya 66 yalitosha kuizamisha Mashetani hao.
Bao la kufuitia machozi la vijana wa Moyes lilifungwa dakika moja baada ya Spurs kupata bao lao la pili kupitia kwa Danny Welbeck.
Kipigo hicho kimeifanya Man Utd iporomoke kutoka nafasi ya sita hadi ya saba na kuipisha Spurs kuwa juu yao kwa tofauti ya pointi tatu.
Spurs ambayo imekuwa na matokeo mazuri tangu ilipomtimua AVB na kupewa Tim Sherwood imekusanya pointi 37 huku Man Utd ikiwa na 34. dakika ya 67. Timu zote zikicheza mechi 20 kila moja.