STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 2, 2015

MALI YAWEKA REKODI AFRIKA YATWAA UBINGWA U17

http://www.foot224.net/wp-content/uploads/2015/03/mali.jpghttp://www.fiba.com/images.fiba.com/Graphic/e7176210/86bb/4e9b/af1c/5e20b580e6d4.jpg?v=20140930135344693MALI imetawazwa kuwa mabingwa wa Afrika kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 17 baada ya kuifunga Afrika Kusini kwa bao 2-0 katika fainali iliyofanyika jijini hapa.
Mabao ya kipindi cha pili yaliyowekwa kimiania na Siaka Bagayoko na Aly Malle yaliiwezesha Mali kutwaa taji hilo.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Mali timu yake ya vijana inayojulikana kama Eaglets kushinda taji la mashindano ya vijana.
Awali, nchi hiyo ilikaribia kushinda taji mwaka 1997, wakati ilipomaliza ya pili nyuma ya washindi Botswana.
Timu zote Mali na Afrika Kusini zilienda katika fainali hiyo ya Jumapili zikiwa tayari zimewahi kukutana katika hatua ya makundi ya mashindano hayo, wakati Afrika Kusini ikiwa nyuma kwa bao 2-0 na kulazimisha sare ya 2-2.
Hatahivyo, Mali haikuruhusu hilo utokea tena, na kuhakikisha inaweka ulinzi mkali baada ya kupata bao la kuongoza na kuhakikisha inaibuka na ushindi.
Bao lao la kwanza lilipatikana baada ya dakika 67 wakati Bagayoko alipofunga kwa kichwa mpira wa kona.
The Eaglets waliongeza bao la pili zikiwa zimebaki dakika 12 kufuatia juhudi binafsi ya Aly Malle. 
Bao hilo alilifunga kutoka umbali wa kama mita 20 kutoka nje ya boksi na kuibua furaha kwa mashabiki wao.
Afrika Kusini walifikiri wangeweza kupata bao la kufutia machozi wakati Khanyisa Eric Mayo alipokaribia kufunga, lakini alijikuta akiwa ameotea.

Jose Mourinho ataka mataji zaidi Stanford Bridge


Mourinhio akilia kwa furaha
Mourinho akikia kwa furaha baada ya kuiwezesha Chelsea kutwaa taji la kwanza msimu huu la Capital One
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedhamiria kutafuta mataji zaidi baada ya kunyakuwa taji la Kombe la Ligi  (Capital One) jana ikiwa ni la kwanza kwa kocha huyo toka achukue mikoba ya kuinoa timu hiyo kwa mara ya pili.
Mabao yaliyofungwa na John Terry na lingine la kujifunga la Kyle Walker yalitosha kuipa ushindi wa mabao 2-0 Chelsea dhidi ya Tottenham Hotspurs katika mchezo wa fainali uliofanyika katika Uwanja wa Wembley. Taji hilo linakuwa la 21 kwa Mourinho toka aanze kufundisha soka.
Akihojiwa Mourinho amesema anajiona kama mtoto aliyeshinda kwa mara ya kwanza kwani mara zote imekuwa ngumu kwake kuishi bila mataji.
Mourinho ambaye kwa mara ya kwanza amewahi kuinoa Chelsea mwaka 2004 hadi 2007 kabla ya kurejea tena mwaka 2013, hilo linakuwa taji lake la saba akiwa timu hiyo na pia kuisaidia Chelsea kulipa kisasi kwa Spurs ambao waliwatungua mabao 2-1 katika fainali za michuano hiyo zilifanyika mwaka 2008.
Kwa furaha kocha huyo alijikuta akimwaga chozi kabla ya baadaye kujumuika na wachezaji wake kushangilia mafanikio hayo yaliyokuja wakati Chelsea ikiongoza msimamo wa Ligi Kuu ya England na pia ikiwa kwenye hatuia nzuri ya kufuzu Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

TAIFA STARS KUPASHA MISULI MOTO COSAFA CUP

TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imethibitisha kushiriki michuano ya kombe la COSAFA nchini Afrika Kusini kufuatia mwaliko wa Baraza la vyama vya soka Kusini mwa Afrika (COSAFA).

Michuano ya kombe la COSAFA inatrajiwa kuanza kutimua vumbi katikati ya mwezi Mei mwaka huu nchini Afrika Kusini, na ratiba ya hatua ya awali ya makundi inatarajiwa kutangazwa leo jioni saa 1:00 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki moja kwa moja na kituo cha runinga cha Supersport 4.

Taifa Stars itakuwa juu (seeded) katika hatua ya makundi, ambapo nchi nane zitagawanya katika makundi mawili na washindi wa kila kundi wataingia hatua ya robo fainali, nchi  nyingine zitakazoanzia kwenye makundi ni Lesotho, Madagascar, Marutius, Namibia, Seychelles, Swaziland.
 
Katika kila kundi, timu zote zitacheza michezo mitatu na mshindi wa kila kundi ataingia katika hatua inayofuata ya robo fainali itakayozijumuisha nchi za  Afrika Kusini, Botswana, Ghana, Malawi, Msumbuji na Zambia ambazo zimeingia katika hatua ya pili kutokana na nafasi zao kwenye msimamo wa viwango vya FIFA.

Kombe la COSAFA lilianza mwaka 1997 linajumuishaa nchi 16 wanchama kutoka Kusini mwa Bara la Afrika, limekua likifanyika kwa kushirikisha nchi wanachama waliopo Kusini mwa bara la Afrika.
Nchi wanachama wa COSAFA ni Afrika Kusini, Angola, Botswana, Comoros, Lesotho, Madagascar, Malawi, Maurtius, Mayotte, Msumbuji, Namibia, Reunion, Sychelles, Swaziland, Zambia na Zimbabwe
.

BASATA LAMLILIA CAPT JOHN KOMBA

Mwili wa Kapteni Komba ukiwasilia Karimjee mapema leo kwa ajili ya kuagwa kabla ya kusafirishwa kwenda kuzikwa kijijini kwao Lutuhi, Nyasa, wilayani Mbinga.
Kapteni John Komba enzi za uhai wake katika picha tofauti akiwajibika katika sanaa yake ya uimbaji wa kwaya
Na Rahim Junior
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limetuma salamu za rambirambi kumlilia Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba aliyefarikia wikiendi iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa yake BASATA imekielezea kifo cha Komba kama pigo kubwa katika tasnia ya sanaa.
Taarifa ya BASATA inasomeka hivi;
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa kifo cha Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Captain John Damian Komba kilichotokea jioni ya Jumamosi ya tarehe 28/02/2015.
Captain John Damian Komba ni msanii na mdau wa muda mrefu wa sekta ya Sanaa nchini. Amekuwa ni taa na nuru ambayo katika kipindi chote cha uhai wake imeangaza na kutoa mwanga angavu kwenye sekta ya Sanaa.
Mchango wake katika muziki wa dansi, kwaya na ule wa kiweledi katika kuandaa na kukuza wasanii mbalimbali nchini hautasahaulika kamwe. Ni mdau aliyeacha alama kuu katika muziki wa bendi, kwaya na taarabu na amejitolea kwa kiasi kikubwa katika kuufikisha muziki wa dansi na kwaya mahali ulipo leo.
Aidha, pamoja na kujiunga na siasa na hatimaye kuwa Mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi, Mheshimiwa Komba hakukoma kuendelea kuipigania sekta ya Sanaa kwani alikuwa ni mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii ambayo kwa mujibu wa kanuni za Bunge ndiyo inayoisimamia na kuishauri Serikali katika masuala yote yahusuyo sekta ya Sanaa na Utamaduni.
Baraza, wasanii na wadau wote wa Sanaa hatuna budi kuendelea kuenzi mema yote aliyotuachia marehemu John Komba hasa katika kutunga nyimbo za hamasa na ujumbe makini na wenye mashiko kwa jamii yote ya Watanzania.
Hakika pengo lililoachwa na Marehemu haliwezi kuzibika, kwani imekuwa ni kama mshumaa uliyozimika ghafla wakati tukiingia kwenye giza.
Baraza linatoa pole kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Anne Makinda, wabunge na wadau wote wa Sanaa hususan wasanii kwa msiba huu. Ni matumaini ya Baraza kwamba, tutaendelea kuenzi mema yote yaliyotendwa na Marehemu, hasa kudumisha upendo na amani katika tasnia yetu ya Sanaa na taifa kwa ujumla.
Bwana ametoa na  Bwana ametwaa, Amen
Godfrey Mngereza
KATIBU MTENDAJI

HII NDIYO NGOMA MPYA YA ALI KIBA-CHEKECHA CHEKETUA

http://api.ning.com/files/3A8rUyA9jKO74o0hv92PLkY4cX5Pc5NkU5Zpw0YYfLFhqQS2Bf6-S-SDS87ET40281CaSxj2VQO9q9KxkyAfyCDor8nBaOVv/IMG_0128.jpg
Baada ya Mwana, Ali Kiba amekuja kivingine na Chekecha Cheketua ebu isikilize hapo chini;

KICHUPA KIPYA CHA ZOLA D FT LATINHO.- I DON'T CARE.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg7q5SJ6OOxchU55rwY3vDndEaHcOnbUOFr39NqBXqkID26wQDFrz9-ALJq1nF84wlrE7ikUfF8CBUSSztJ9iU-jbHvzB2MaIa1ewh5SeXh2jnVFik3CQJSYaNPJEz7e2kT2MH0n6wenu8/s1600/Zola+D2.JPG
Zola D King aliyeachia video ya wimbo wake wa I Don't Care

Sunday, March 1, 2015

CHELSEA, SPURS KATIKA FAINALI YA KISASI

KLABU za Chelsea na Tottenham Hotspur zinatarajiwa kuvaana leo katika pambano la kisasi la fainali za Kombe la Ligi (Capital One).
Pambano hilo litakalochezwa kwenye uwanja wa Wembley linarejesha mchezo wa fainali za mwaka 2008 ilizozikutanisha timu hizo kwenye uwanja huo na Spurs kuitambia Chelsea kwa mabao 2-1.
Katika pambano hilo lililochezwa Februari 24, 2008, Spurs ilinyakua taji hilo katika muda wa nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika kwa timu hizo kufungana bao 1-1 Chelsea wakitangulia kabla ya Spurs kurejesha.
Kadhalika pambano hilo la Fainali hizo za Kombe la Ligi limekuja ikiwa ni wiki kadhaa tangu Spurs walipoitoa nishai Chelsea kwa kuichapa mabao 5-3 katika pambano la marudiano ya Ligi Kuu ya England.
Awali Spurs ilicharazwa mabao 3-0 nyumbani kwa Chelsea mwaka uliopita na waliporudiana White Hart Lane waliwashughulikia Chelsea jambo linalofanya mechi ya leo kujaa visasi vitupu.
Chelsea chini ya Jose Mourinho itawakosa baadhi ya nyota wake akiwamo Nimanja Matic aliyefungiwa mechi mbili baada ya kupungiwa adhabu na FA kwa kadi nyekundu aliyoipata wiki iliyopita.
Hata hivyo timu hiyo inapewa nafasi kubwa ya kuwatambia wapinzani wao ambao wanauguza machungu ya kung'olewa kwenye michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europa League) na Fiorentina ya Italia.
Ikiwa na wakali kama Ces Fabrigas, Diego Costa, Eden Hazard, Willian na wengine, Chelsea itapenda kutwaa taji hilo ili kuweka hazina kwa msimu huu baada ya awali kutolewa katika Kombe la FA.
Vinara hao wa Ligi Kuu wanapaswa kuwa makini na kinda linalotisha Harry Kane ambaye amekuwa wakiwaliza makipa hodari kama alivyoonya kipa wa Chelsea, Thibaut Courtois.
Rekodi zinaonyesha kuwa timu hizo zimeshakutana mara 134, Chelsea ikishinda mara 57 na wapinzani wao mara 44 na mechi 33 zikiisha kwa sare na pambano la leo litakuwa la 135 kwao katika michuano yote.
Je, ni Chelsea au Spurs atakayecheka leo katika uwanja wa Wembley? Bila shaka ni suala la kusubiri kuona ila kwa hakika ni bonge la mechi.

Arsenal, Manchester City vitani tena EPL

WAKIWA na maumivu ya vipigo walivyopata kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, klabu za Arsenal na Manchester City zitakuwa tena vitani leo kwenye viwanja tofauti katika Ligi Kuu ya England (EPL).
Arsenal walikandikwa mabao 3-1 na Monaco ya Ufaransa itakuwa nyumbani kuumana na Everton, wakati Manchester City watakuwa wageni uwanja wa Anfield kupepetana na Liverpool.
Mabingwa watetezi hao walikumbana na kipigo cha mabao 2-1 nyumbani dhidi ya Barcelona, na leo watakuwa na kazi ngumu mbele ya Liverpool ambayo imekuwa na matokeo ya kuvutia siku za karibuni.
Katika mechi nne zilizopita za ligi hiyo, Liverpool haijapoteza mchezo wowote, pia ikishinda katika Kombe la Ligi na Ligi Ndogo ya Ulaya.
Zilipokutana mara ya mwisho Agosti 25 mwaka jana katika mechi ya mkondo wa kwanza Liverpool ilinyooshwa na Manchester City kwa mabao 3-1 ugenini hivyo leo kulazimika kulipa kisasi kwa wageni wao.
Kocha wa Man City, Manuel Pellegrini amesisitiza umuhimu wa kupata ushindi katika mchezo huo wa ugenini ili kuweza kupunguza pengo la pointi dhidi ya Chelsea wanaoongoza msimamo wakiwa na pointi 60.
Katika mechi itakayochezwa Emirates, Arsenal itavaana na Everton ambayo katika mechi yao ya kwanza iliyochezwa Agosti 23 mwaka timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kutosa sare ya mabao 2-2.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger aliyewashutumu vijana wake kwa kipigo cha Monaco atakuwa na kazi ngumu ya kuwaongoza kikosi chake kupata ushindi nyumbani ili angalau kuwafukuzia Man City.
Wenger anatambua ni michuano miwili tu mpaka sasa ndiyo wana hakika ya kutwaa taji kama watakomaa, Kombe la FA wanaotetea na watakaovaana naManchester United wiki ijayo na michuano ya ligi.
Nafasi ya kusonga mbele katika Ligi ya Mabingwa Ulaya ni finyu baada ya kipigo cha Monaco wakilazimika kuhakikisha wapate ushindi wa 3-0 wiki mbili zijazo nchini Ufaransa.
Everton wenyewe wamekuwa na mwenendo wa kuchechemea msimu huu, ingawa siyo timu ya kubezwa kwani inaweza kufanya lolote katika pambano hilo la leo.