STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Waislam wakiungana na wenzao ulimwenguni kuswali Eid El Hajj leo

Waumini wa Kiislam wakisikiliza hotuba mbili za Eid el Hajj leo asubuhi
Sheikh akitoa hotuba baada ya sala ya eid leo
Waumini wakiwa katika iktidar wakati wa Swala ua Eid leo
Waumini wakisudu katika swala la Eid iliyoswaliwa viwanja vya Jangwani na maeneo mengine pamoja na misikiti kadhaa inayofuata kalenda ya Kiislam ambapo leo inaoonyesha ni Mwezi 10 Mfungo Tatu
WAUMINI wa kiislam wa nchini Tanzania leo wameungana na waumini wengine wa dini hiyo duniani kuswali swala ya Eid El Hajj kuashiria kumalizika kwa ibada ya Hijja ambapo Mahujaji leo wanachinja wanyama baada ya jana kusimama Arafa.
Karibu dunia nzima wapo katika shamrashamra hizo za Eid tofauti na hapa Tanzania ambapo baadhi wanakusudia kusherehekea kesho kwa mujibu wa Baraza Kuu la Kiislam Tanzania (BAKWATA) waliowatangazia waumini Eid ni kesho Jumatano...! MICHARAZO iunawatakia waumini woite Eid Njema Inshallah.

Maiti yafukuliwa kaburini na kukatwa kichwa Geita

Picha hii haihusiani na kaburi lililofukuliwa Geita




WATU wasiofahamika huko Geita wamelifukua kaburi na mwanaume mmoja kisha kukata kichwa cha maiti yake na kutowekwa na kichwa hicho kusikojulikana.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoifikia MICHARAZO, zinasema kuwa watu hao wanadaiwa kuyfanya unyama huo usiku wa kuamkia jana majira ya usiku kwa kulifukua kaburi la mtu huyo ambaye hakuweza kufahamika kisha kupasua sanduku alilozikiwa na kukata kichwa cha maiti hiyo na kutoweka na kichwa hicho.
Mashuhuda wanasema tukio hilo liligundulika jana wakati wachimba makuburi walipoenda katika makaburi hayo na kukuta kaburi hilo likiwa limefukuliwa na huku jeneza likiwa lipo juu yake likiwa limepasuliwa na walipoangalia ndani wakashangazwa kukutwa mwili huo ukiwa hauna kichwa.
Inaelezwa maiti hiyo ilizikwa miezi mitatu iliyopita na baadhi ya watu wamehusisha na vitendo vya kishirikina kwani silo jambo la kawaida maiti kufukuliwa kisha kukatwa kichwa hivi hivi tu.
Jeshi la Polisi mkoani Geita limethibitisha juu ya tukio hilo na kwamba wanafanya upelelezi juu ya watu waliohusika kufanya unyama huo.