STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Maiti yafukuliwa kaburini na kukatwa kichwa Geita

Picha hii haihusiani na kaburi lililofukuliwa Geita




WATU wasiofahamika huko Geita wamelifukua kaburi na mwanaume mmoja kisha kukata kichwa cha maiti yake na kutowekwa na kichwa hicho kusikojulikana.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoifikia MICHARAZO, zinasema kuwa watu hao wanadaiwa kuyfanya unyama huo usiku wa kuamkia jana majira ya usiku kwa kulifukua kaburi la mtu huyo ambaye hakuweza kufahamika kisha kupasua sanduku alilozikiwa na kukata kichwa cha maiti hiyo na kutoweka na kichwa hicho.
Mashuhuda wanasema tukio hilo liligundulika jana wakati wachimba makuburi walipoenda katika makaburi hayo na kukuta kaburi hilo likiwa limefukuliwa na huku jeneza likiwa lipo juu yake likiwa limepasuliwa na walipoangalia ndani wakashangazwa kukutwa mwili huo ukiwa hauna kichwa.
Inaelezwa maiti hiyo ilizikwa miezi mitatu iliyopita na baadhi ya watu wamehusisha na vitendo vya kishirikina kwani silo jambo la kawaida maiti kufukuliwa kisha kukatwa kichwa hivi hivi tu.
Jeshi la Polisi mkoani Geita limethibitisha juu ya tukio hilo na kwamba wanafanya upelelezi juu ya watu waliohusika kufanya unyama huo.

No comments:

Post a Comment