STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Ghana yaikoboa Misri 3-1 ni mapumziko kwa sasa

StarAfrica
Ghana-Black Stars

MABINGWA wa zamani wa Afrika Ghana, ikiwa nyumbani mpaka sasa wakati wa mapumziko inaoongoza kwa mabao 3-1 dhidi na Mafarao wa Misri katika pambano la awali la hatua ya mwisho ya mtoano kuwania Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2014.
Mkali Asamoah Gyan alianza kuwashtua mabingwa wa kihistoria wa Afrika, Misri kwa bao la dakika nne kabla ya beki wa Misri Wael Gomma kujifunga bao katika harakati za kuokoa mpira uliopigwa na Michael Essien na kuipa Ghana uongozi wa mabao 2-0 kwenye dakika ya 22.
Hata hivyo mkongwe Mohammed Aboutrika aliipunguza machungu kwa kufunga bao la Misri kwa mkwaju wa penati dakika ya 41 kabla ya Abdulmajed Waris kufunga bao la tatu dakika moja kabla ya mapumziko.
Tutaendelea kuwaletea matokeo juu ya mpambano huo,. licha ya kufahamu wapo wengine wanaoufuatilia 'live' kupitia kwenye runinga.

No comments:

Post a Comment