STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Safina wa Mizengwe aing'ata serikali sikio

Safina wa Mziengwe
MCHEKESHAJI mahiri wa kike anayetamba kupitia kipindi cha vichekesho cha Mizengwe, Jesca Kindole 'Safina' ameitaka serikali na wadau wa sanaa nchini kuongeza juhudi katika kudhibiti vitendo vya wizi wa kazi za wasanii ili kuwasaidia kunufaika na kazi zao.
Safina alisema mbali na sanaa kuwa moja ya ajira tegemeo kwa watu wengi, lakini kama ingetengenezewa mazingira mazuri ingeiwezesha serikali kuvuna pato la kutosha kuliko ilivyo sasa ambapo linaishia mikononi mwa wachache.
Msanii huyo alisema wasanii wengi wa Tanzania wanaishi kimaskini kutokana na kufanyiwa 'uharamia' na unyonyaji mkubwa, kitu ambacho imefika wakati serikali na wadau wanaosimamia fani hiyo kutoa makucha.
"Sanaa inalipa sana Bongo, ila wizi na unyonyaji uliopo unatufanya wasanii wengi kuishi maskini tofauti na jasho tunalolitoa, pia serikali inapoteza mapato mengi kupitia huko, sasa ni wajibu wao kuamka na kuikomalia," alisema.
Mchekeshaji huyo anayejiandaa kutoka na filamu ya 'Kijiji Chetu', alisema anaamini kama tasnia ya sanaa itatengenezewa mazingira mazuri, wasanii nchini wataishi maisha mazuri kama wa mataifa mengine.

No comments:

Post a Comment