STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Misri yatunguliwa bao la sita, Ghana yanusa fainali za Kombe la Dunia

Asamoah Gyan and  Wael Gomaa

MAFARAO wa Misri imeendelea kufa mjini Kumasi baada ya muda mchache uliopita wakitunguliwa bao la sita na Ghana katika pambano lao la awali la hatua ya mwisho ya mchujo wa Fainali za Kombe la Dunia kwa Bara la Afrika.
Pamoja na kufanya mabadiliko ya kuwaingiza akina Tshabalala, Misri wamepotea kabisa kwa wewnyeji ambao wanacheza watakvyo wakiwa na uhakika kwa asilimia kubwa kutinga fainali hizo za WC za 2014 zitakazofanyika Brazili.
Bao hilo la sita limetupiwa kimiani na Christian Atsu dakika ya 89 na kuonyesha dhahiri Ghana imeshaingiza mguu mmoja katika fainali hizo licha ya kwamba pambano lao la marudiano baina yao litafanyika Nov. 19.
Game ishaisha na Misri kuwa na kibarua cha kushinda nyumbani kwao mechi ya marudiano kwa mabao 5-0?! Tusubiri tuone!

No comments:

Post a Comment