STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Golden Bush yaifyatua Pugu Veterani 1-0

Golden Bush Veterani

ILE timu ya Veterans isiyofungika hapa Dar es Salaam na mikoa ya jirani ilitoa kipigo cha goli dhidi ya wanzetu Pugu Veterans. Goli liliwekwa wavuni Said Swedi baada ya kuna safi kabisa iliyopigwa na Shomari Pengo. Goli hili lilipatikana kipindi cha kwanza mara baada mashambulizi ya haraka haraka yakiongozwa na beki za kupanda na kushuka zikiongozwa na Shadrack Nsajigwa, Faraj huku kiungo kikikamatwa barabara na Ticotico akishirikiana na Said Sued 'Panucci'. Kama si uhodari wa kipa wa Pugu basi Golden Bush tungeibuka na goli zaidi ya 5. Hata hivyo matokeo tumeyafurahia kwasababu tumepata ushindi ambao ulikuwa na walazima.
Kesho Golden Bush tutakuwa Stakishari kwa mualiko wa Stakishari Veterans kucheza mechi ya kirafiki na kusherekea sikukuu pamoja na wenzetu. Baada ya sikukuu timu yetu itaelekea Zanzibar kwa mechi za kirafiki ili kufanya maadalizi ya mwisho kabisa ya gemu yetu ya kufunga mwaka dhidi ya Wahenga. Game hii uwa inakusanya wakazi wote wa Sinza na sehemu mbalimbali za jirani hivyo tunalazimika kufanya maandalizi ya nguvu sana.
Tuko kwenye mchakato wa kuomba udhamini wa game hiyo ya kufunga mwaka, tunashukuru mungu big Companies ambazo zitambua ushawishi mkubwa wa game hii zimeshaonyesha nia ya kutaka kutudhamini na kufunya matanagazo kwa kutumia wachezaji wengi maarufu wanaounda vikosi hivi viwili yaani Wahenga na Golden bush Veterans.

Asanteni
Onesmo Waziri 'Ticotico' Mchezaji Mwandamizi Golden Bush FC.

No comments:

Post a Comment