STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Neymar aiongoza Brazil kuizima Zambia

Prediksi Skor Brasil vs Zambia 15 Oktober 2013
MABINGWA wa zamani wa Afrika, Zambia leo imekiona cha moto baada ya kutandikwa mabao 2-0 na wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia za mwakani Brazil katika pambano la kirafiki la kimataifa lililochezwa Beijing China.
Mabao ya kipindi cha pili kutoka kwa mtokea benchi Oscar katika dakika ya 59 akimalizia pasi murua ya Paulinho na Dede kuongeza jingine dakika ya 66 kwa pasi ya nyota mpya wa Barcelona, Neymar yaliizamisha Zambia ambayo imeondokewa na kocha wake  Herve Renard aliyeteuliwa kuinoa timu ya darajha la kwanza ya nyumbani Ufaransa.
Zambia ilicheza ikiwa na kocha wake mpya, Mfaransa mwingine Patrice Beaumelle.

Katika mechi nyingine; Korea ya kaskazini imeitungua Mali mabao 3-1, huku Japan ikilala 1-0 kwa Belarus, Ufilipino ikiitafuna Pakistan mabao 3-1.


No comments:

Post a Comment