STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

Jahazi la Misri lazidi kuzama, Gyan atupia bao jingine

Asamoah Gyan and  Wael Gomaa
Gyan akichuana na Wael Gomma

JAHAZI ya mafarao wa Misri linazidi kuzama baada ya muda mfupi uliopita Asamoah Gyan kutupia bao jingine la nne kwa Ghana wakati mchezo ukiingia dakika ya 60 hivi sasa.
Gyan katupia bao hilo la pili kwake katika mchezo huo unaochezwa mjini Kumasi katika dakika ya 54.
Hivi punde tena Ghana imepata bao la tano kupitia Sulley Muntari katika dakika ya 73kwa mkwaju wa penati, kuonyesha imepania kuidhiri Misri ambayo imekuwa ikiinyanyasa kila inapokutana nayo ambapo katika mechi 18 za awali za kukutana kwa timu hizo Ghana imeshinda mara nne na kufungwa 9 huku michezo mitano ikiisha kwa sare.

No comments:

Post a Comment