STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 24, 2013

Real Madrid yaijibu Barca, Atletico Madrid ikifanya kufuru La Liga

Fabregas akifunga mkwaju wake wa penati jana
Ronaldo akielekea kufunga bao la kwanza la Real Madrid kabla ya kutolewa kwa maumivu
Teamwork: Neymar and Marc Batra celebrate with the former Arsenal midfielder
Barca wakipongezana
RAUL GARCIA KOKE ATLETICO MADRID GETAFE LIGA BBVA 11232013
Villa na Garcia wa Atletico Madrid wakishangilia mabao yao ya jana. Kila mmoja kati ya wawili hao alifunga mabao mawili
WAKATI Real Madrid ikijibu mapigo kwa mahasimu wao Barcelona waliotangulia kushinda mabao 4-0 kwa kuichakaza Almeria kwa magoli 5-0, Atletico Madrid ilifanya kufuru zaidi kwa kutoa kisago cha mabao 7-0 katika Ligi ya Hispania.
Madrid ilipata ushindi huo ugenini kupitia kwa mabao ya Cristiano Ronaldo aliyefunga bao la mapema la dakika ya tatu tu ya mchezo kabla ya kutolewa uwanjani kwa kuumia.
Mabao mengine yalifungwa na Karim Benzema dakika ya 61 pasi ya Jese Rodriguez kabla ya Gareth Bale kufunga bao la tatu dakika ya 71,  Isco akaongeza la nne na Alvaro Morata akahitimisha karamu ya mabao dakika ya 81.
Mapema Barcelona waliifumua timu ya Grenada kwa mabao 4-0 bila ya kuwa na nyota wake, Lionel Messi aliye majeruhi.
Magoli ya penati ya Andres Iniesta na nahodha wa zamani wa Arsenal, Cesc Fabregas yaliipa uongozi Barcelona kabla ya kuongeza mengine mawili kupitia kwa Alex Sanchez na Pedro kuifanya Barca iendeleze rekodi ya kushinda mechi mfululizo.
Hata hivyo ni Atletico Madrid walifanya kufuru usiku wa manane wa leo baada ya kuifumua Getafe kwa mabao 7-0 na kuzidi kung'ang'ania katika nafasi ya pili ya msimamo wa La Liga ikifikisha pointi 37,
Raul Garcia na David Villa walifunga mara mbili, huku Diego Costa, Adrian na lile la kujifunga la Lopo lilitosha kuifanya Atletico kuifukizia Barca inayoongoza kwa pointi 40, tatu pungufu na ilizonazo klabu hiyo.

Saturday, November 23, 2013

TFF yaunda kamati zake ndogondogo, Zitto Kabwe, Wilfred Kidao waula

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametangaza wajumbe wa kamati ndogongo (standing committees) wakati zile za haki (judicial organs) na uchaguzi zitaundwa baadaye.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika leo (Novemba 23 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, Rais Malinzi alisema kamati hizo zimeundwa kwa mujibu wa katiba ili kuisaidia Kamati ya Utendaji.

Pia ametangaza wajumbe wanne wa Kamati ya Utendaji aliowateua. Wajumbe hao ni Richard Sinamtwa na Ramadhan Nassib, wakati wengine wanaoingia moja kwa moja kwenye Kamati ya Utendaji kutokana na kamati wanazoziongoza ni Dk. Paul Marealle na Saloum Umande Chama.

Kamati ya Fedha na Mipango inaongozwa na Makamu wa Rais wa TFF, Wallace Karia wakati wajumbe ni Francis Ndulane (Makamu Mwenyekiti), Omari Walii, Eliud Mvella, Said Muhammed, Geofrey Nyange, Kidao Wilfred, Ayoub Nyenzi, Lina Kessy na Cyprian Kuhyava.

Geofrey Nyange anaongoza Kamati ya Mashindano wakati wajumbe ni Clement Sanga (Makamu Mwenyekiti), Msafiri Mgoyi, James Mhagama, Mohamed Nassoro, Moses Katabaro, Seif Ahmed, Gerald ambi, Davis Mosha, Said George na Nassoro Idrissa.

Kinara wa Kamati ya Ufundi ni Kidao Wilfred wakati wajumbe ni Athumani Kambi (Makamu Mwenyekiti), Vedstus Lufano, Blassy Kiondo, Rahim Kangezi, Patrick Kahemele, Daud Yassin, Nicholas Mihayo na Dk. Cyprian Maro.

Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana inaongozwa na Ayoub Nyenzi, Khalid Abdallah (Makamu Mwenyekiti), Ali Mayay, Mulamu Ng’hambi, Apollo Kayungi, Said Tully, Luteni Kanali Charles Mbuge, Lameck Nyambaya na Ibrahim Masoud.

Lina Kessy anaongoza Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake wakati wajumbe ni Shyrose Bhanji (Makamu Mwenyekiti), Zena Chande, Amina Karuma, Dk. Cecilia Makafu, Zafarani Damoder, Beatrice Mgaya, Sofia Tigalyoma, Martin Mung’ong’o na Engrid Kimaro.

Kamati ya Waamuzi inaongozwa na Saloum Umande Chama, Nassoro Said (Makamu Mwenyekiti), Charles Ndagala (Katibu), Riziki Majala, Kanali Isaro Chacha, Paschal Chiganga, Victor Mwandike, Soud Abdi na Zahra Mohamed.

Hamad Yahya Juma ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi anaongoza Kamati ya Habari na Masoko wakati wajumbe ni Naibu Waziri January Makamba (Makamu Mwenyekiti), Tido Mhando, Yusuf Manji, Yusuf Bakhresa, Samwel Nyalla, Jack Gotham, Fredrick Mwakalebela na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA).

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji inaongozwa na Richard Sinaitwa, Moses Karuwa (Makamu Mwenyekiti), Zacharia Hanspoppe, Hussein Mwamba, Philemon Ntahilaja, Abdul Sauko na Imani Madega.

Kiongozi wa Kamati ya Ukaguzi wa Fedha ni Ramadhan Nassib wakati wajumbe ni Zitto Kabwe (Makamu Mwenyekiti), Nicholas Magarinza, Jackson Songora, Epaphra Swai, Kalilo Samson, Goodluck Moshi, Golden Sanga na Elias Mwanjala.

Dk. Paul Marealle anaongoza Kamati ya Tiba wakati wajumbe ni Dk. Fred Limbanga (Makamu Mwenyekiti), Dk. Mwanandi Mwankemwa, Dk. Nassoro Matuzya, Dk. Eliezer Ndelema na Asha Sadick.

TFF yamrejesha Rage madarakani yamtaka aitishe mkutano wa dharura

Rais wa TFF, Jamal Malinzi aliyetoa taarifa za Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage aitishe mkutano haraka baada ya awali kupiunduliwa na wajumbe wa kamati ya utendaji ya klabu yake akiwa nje ya nchi
MWENYEKITI  wa Simba, Ismail Aden Rage ameagizwa kuitisha Mkutano Mkuu wa Dharura wa klabu ndani ya siku 14 kuanzia sasa.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa agizo hilo baada ya kubaini kuwa mgogoro katika klabu baada ya kupokea barua mbili; moja kutoka Kamati ya Utendaji ikielezea kumsimamisha uongozi Rage, na nyingine kutoka kwa Mwenyekiti huyo ikielezea kutotambua kusimamishwa huko.

Uamuzi wa TFF umefanywa kwa kuzingatia Ibara ya 1(6) ya Katiba ya Simba inayosema: 
 
“Simba Sports Club ni mwanachama wa TFF, itaheshimu Katiba, kanuni, maagizo na uamuzi wa TFF na FIFA, na kuhakikisha kuwa zinaheshimiwa na wanachama wake.”

TFF itatuma wawakilishi wake katika mkutano huo, na kumuagiza Mwenyekiti wa Simba kuhakikisha wanachama wote wenye hoja wanapata fursa ya kusikilizwa.

Mahafali ya Tano ya Kidato cha Nne Mwandege Boy's yalivyofana leo Mkuranga

Wanafunzi waliosalia shuleni wakisimama kumpokea mgeni rasmi
Hata wazazi na walezi nao walisimama wima
Pre Form One nao walikuwapo katika mahafali hayo
Wanafunzi wa kidato wa tatu wakionyesha onyesho la lugha ya Kiswahili kusherehesha mahafali hayo ya leo
Baadhi ya wahitimu wa Kidato cha nne wakiwa wametulia vitini
Mwandege Boys kuna vipaji vya uigizaji usipime!
Yaani ni Full Kidigitali Mwandege Boys
Igizo likiendelea kuhusiana na umuhimu wa kuzingatia masomo shuleni
Hata Bongo Movie hawaoni ndani kwa madogo hawa, vipaji vitupu
Wahitimu wa kidato cha Nne Jesse na Godwin wakisoma taarifa ya habari hawa jamaa nouma

Hashim Abdallah (kulia) akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wa kidato cha nne

Wanafunzi wa kidato cha nne wakitumbuiza
Leo tunawaaga kwaherini tuliwazoea kaka zetu, ndivyo wanavyoimbiwa wahitimu waliokaa na wanafunzi wenzao wa kidato cha tatu
Yaani ni full burudani


Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mhe. Mercy Silla (wa pili kulia) akiwasili eneo la tukio akisindikizwa na Mkuu wa Shule, Mwl Enock Walter (kulia)


Meza kuu ikishuhudia vipaji vya wanafunzi wa Mwandege Boys Sec
Mashairi nayo yalisomwa kuwaaga wahitimu
Mmoja wa wazazi akitoa nasaha zake

Mzazi wa kiume naye alitoa nasaha zake.
Mkuu wa Shule ya Mwandege Boys, Mwl Enock Walter akisoma risala

Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mercy Sillah akisoma risala yake ambapo aliwataka wahitimu kutojiingiza kwenye kishawishi cha biashara za dawa za kulevya kwa nia ya kutaka utajiri wa haraka badala yake wakomalie kujiendeleza kimasomo na kutumia vipaji walivyonayo kujiletea mafanikio maishani mwao.
Mgeni rasmi (kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwandege, Joseph Awino sehemu ya vitabu vilivyotolea na uongozi wa Shule ya Mwandege Boys kwa shule hiyo ya msingi ili kusaidia kukuza taalum

Mwanafunzi wa Pre Form One, Benard Deogratius aliyefanya vizuri katika masomo yake hayo akikabidhiwa zawadi na Mgeni rasmi

Mhitimu akikadhiwa cheti chake
 

Hata walimu nao walitunukiwa vyeti kwa kufanya vyema shuleni MwandegeBoys Sec

Mmoja ya wahitimu akikabidhiwa cheti na DC Mercy Sillah

Friday, November 22, 2013

Maguli aomba sapoti nje ndani Kili Stars ibebe Chalenji Kenya

Elias Maguli
MSHAMBULIAJI mpya na chipukizi wa timu ya taifa ya Kilimanjaro Stars, Elias Maguli, amewaomba watanzania waliopo Kenya na wale wa nyumbani Tanzania kuwaunga mkono katika ushiriki wao wa michuano ya Kombe la Chalenji inayoanza Jumatano nchini humo.
Maguli alisema kwa watanzania wanaobaki nyumbani waiunge mkono timu hiyo kwa kuiombea dua na kuifanyia maombi, huku wale wa wanaishi Kenya kujitokeza kwa wingi uwanjani kuwashangili ili timu hiyo ifanye vyema katika michuano hiyo inayoshirikisha timu za nchi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Akizungumza na MICHARAZO mchana huu katika mahojiano maalum, Maguli anayeichezea Ruvu Shooting na kushika nafasi ya pili katika orodha ya wafungaji wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu, alisema bila kuungwa mkono ni vigumu Kili Stars kufanya vyema katika michuano hiyo.
Maguli alisema wachezaji wa kikosi hicho kinachotarajiwa kuondoka Jumatatu kabla ya Alhamisi kuwavaa Chipolopolo ya Zambia wamejiandaa vya kutosha kuwapa raha watanzania kutokana na maandilizi waliyofanya chini ya kocha wao, Kim Poulsen, lakini sapoti ya mashabiki ni muhimu.
"Wachezaji tumejiandaa vya kutosha kutowaangusha watanzania, nasi tunaomba tuungwe mkono kwa wlaiopo Kenya wajitokeze uwanjani na wale wa nyumbani watuunge mkono kwa sala na maombi na hatimaye tutarejea na kikombe Mungu akipenda," alisema.
Kuhusu kuwemo kwenye kikosi hicho cha Kili Stars, Maguli alisema anajisikia fahari kwa kuwa Tanzania ina wachezaji bora na nyota lakini kocha amemuona anastahili kuiwakilisha nchi na atapigana kiume akishirikiana na wenzake ili kuipa timu hiyo taji lake la nne.
Tanzania Bara imenyakua ubingwa wa michuano hiyo mwaka 1974, 1994 na 2010 na mara nyingine zote tangu michuano hiyo ianze kutambuliwa kama Chalenji miaka 40 iliyopita imekuwa kama msindikizaji tu.

Breaking Newzz: Zitto Kabwe apigwa 'stop' CHADEMA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhIWLSkbykk_sjO3i9lNEUs2svxN7oCsv5Vbr-4u7kxDo_t6240fLBSEFxdQguEQHn_YHmZqr182kNLPNwkv8REW_MaB8TqVLjt_8pgK5wCwBi1YPChOby84dZbTcwqj3D90RVMlZpRUKc/s1600/chadema.jpg
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeeman Mbowe akizungumza kwenye kikao hicho (Picha:CHADEMA Blog)
TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa CHADEMA kimeamua kumsimamisha na kumvua nyadhifa zote aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wake na Mbunge wa Kigoma Kaskazini na wamempa muda wa saa 78 kujieleza kwa nini asifukuzwse chamani kimoja.
MICHARAZO inafuatilia kwa kina na itawafahamisha, hii ni ikiwa ni maamuzi ya kikao cha Kamati kuu ya chama hicho kilichoanza kukutana tangu juzi.

Nyilawila awashukia mabondia wenzake wanaendekeza wanga

BONDIA Kalama Nyilawila 
BONDIA  Karama Nyilawila amewataka mabondia wa Tanzania kuacha imani
za kishirikina na badala yake wafanye mazoezi  ili waweze kufikia mafanikio.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Nyilawila alisema  hapendezwi na
vitendo hivyo kwani vinauwa viwango vya michezo nchini.
Alisema mabondia wanatakiwa wasiamini kabisa na kwamba wamekuwa
wakifanya mambo hayo wanapoenda kupambana nje ya nchi.
Nawasihi waachane na imani za kishirikina kwani wanapokwenda huko
huishia kupigwa kwa KO ila naamini wakizingatia mazoezi yatawasaidia
kufanya vema,"alisema.
Alisema mazoezi pekee ndiyo yatakayomsaidia bondia kushinda pambano
lake na si kwenda kwa mganga na kumpa nguvu za giza na badala yake
jitihada zake binafsi  ulingoni ndizo zitakazomfaa.
Alisema watu wasitafute mchawi  aliyesababisha Tanzania isifanye vema
kimataifa kwani wachawi ni wanamichezo wenyewe na wengi wamekuwa
wakiamini imani hizo.
Nyilawila alisema kwa sasa yupo katika mazoezi makali chini ya meneja wake
Seleman Zugo na kwamba  amejipanga kushinda mapambano yake yote yaliyopo mbele yake kwa KO raundi za mwanzoni ambambo hivi karibuni bondia huyo alimshinda kwa KO  ya raundi ya kwanza bondia Kaminja Ramadhani mpambano ulioandaliwa na Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi  Rajabu Mhamila 'Super D' uliofanyika Novemba 10 jijini Dar es Salaam.

Thursday, November 21, 2013

Simanzi tupu rufaa ya Babu Seya

MSANII JOSEPH MARA AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA KUTOLEWA HUKU NA KUTUPILIA MBALI
WATU MBALIMBALI PAMOJA NA JAMAA ZAO WAKICHUNGULIA KWENYE  CHUMBA CHA MAHAKAMA MARA BAADA YA KUTUPILIA MBALI KWA KUTUMIA MLANGO WA VIOO
BAADHI YA NDUGU WAKILIA WAKATI NGUZA NA  MWANAE WAKIPANDA GARI LA MAGEREZA LEO
BAADHI YA NDUGU WAKILIA WAKATI NGUZA NA  MWANAE WAKIPANDA GARI LA MAGEREZA LEO
BAADHI YA NDUGU WAKILIA WAKATI NGUZA NA  MWANAE WAKIPANDA GARI LA MAGEREZA LEO
BAADHI YA WATU MBALIMBALI WALIOFIKA KATIKA MAHAKAMA YA RUFAA LEO
NDUGU NA JAMAA WAKILIA KWA HUZUNI KATIKA MAHAKAMA HIYO LEO
BAADHI YA NDUGU WAKIMUAGA NGUZA VIKING NA MWANAE JOHNSON NGUZA 'PAPII KOCHA'
WANAMUZIKI NGUZA VIKING NA JOHNSON NGUZA 'PAPII KOCHA'  WAKIWAAGA NDUGU NA MASHABIKI NA JAMAA WALIOFIKA KWENYWE MAHAKAMA YA RUFAA LEO BAADA YA KUTUPIWA MBALI

WAKIPANDA KWENYE GARI LA MAGEREZA

WATUI MBALIMBALI PAMOJA NA JAMA WAKIMUAGA BABU SEYA WAKATI GARI LA MAGEREZA LIKONDOKA LEO MAHAKAMA YA RUFAA

WAKIPANDA KWENYE GARI LA MAGEREZA

WAKITOKA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKAMA YA RUFAA LEO

BAADHI YA JAMAA ZAO WAKILIA HUKU WAKIWAPIGIA SIMU JAMAA ZAO LEO