STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 11, 2014

Rooney katuponza kwa Bayern-MOyes

Wayne Rooney
KOCHA David Moyes amekiri kwamba alifanya makosa makubwa kumharakisha Wayne Rooney kurejea uwanjani katika kikosi cha Manchester United kilicholala 3-1 dhidi ya Bayern Munich katika mechi yao ya marudiano ya robo fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya England, ambaye aliumia wiki iliyopita, alipasishwa kuchukua namba yake katika kikosi cha kwanza cha Man U, lakini hakuweza kuwasaidia Mashetani Wekundu wasikumbane na kipigo hicho kwenye Uwanja wa Allianz Arena.
"Kuna wakati nilihisi kwamba anashindwa hata kupiga mpira lakini yeye ni mchezaji muhimu sana kwetu," Moyes aliwaambia waandishi wa habari. "Sikujiwa na fikra kwamba tumeshatoka mchezoni, daima niliamini kwamba tulikuwa na nafasi ya kusonga mbele.
"Ilipokuwa 2-1 tulihitaji kufunga moja ili tuwe 2-2, lakini mambo hayakutuendea vyema. Nadhani ilikuwa ni kukosa bahati kulikotufanya tukafungwa bao lile la tatu.”

Ruvu Star sasa wana Kioo na Facebook

Rogart Hegga 'Katapila' mmoja wa viongozi na waimbaji wa Ruvu Star
BENDI ya muziki wa dansi ya Ruvu Stars ya Mlandizi Pwani wapo studio kwa ajili ya kumalizia nyimbo zao tatu za mwisho kukamilisha albamu ya kwanza.
Mmoja wa viongozi wa bendi hiyo, Rogart Hegga 'Katapila' alisema nyimbo hizo zimetungwa na waimbaji watatu tofauti ukiwamo unaitwa 'Kioo' ambao ni utunzi wa kiongozi mkuu wao, Khamis Kayumbu 'Amigolas'.
Alizitaja nyimbo mbili za mwisho kuwa ni 'Chewa Original' wa Seleman Muhumba na 'Facebook' wa Mkuu wa Jukwaa, Victor Mkambi ambaye pia ni mpapasa kinanda mahiri nchini.
"Tunamalizia nyimbo zetu tatu za mwisho kukamilisha albamu kabla ya kuanza maandalizi ya uzinduzi wa bendi na albamu hiyo, pia tumesaini mkataba na kampuni ya kurekodi video ya albamu hiyo."
Aliongeza, video hiyo inatarajiwa kuanza kurekodiwa wiki ijayo kwa  nyimbo tatu za awali ambazo ni; 'Spirit' alioutunga yeye (Hegga), 'Network ya Mapenzi' wa Toto Tundu na 'Jua Kali' wa Kuziwa Kalala.
"Video hiyo itaanza na nyimbo za awali tulizotambulisha kwa mashabiki na tukimalizia hizi tunazorekodi tutahimisha albamu na ndipo mipango ya uzinduzi," alisema.
Alisema bendi yao ipo hatua ya mwisho kabla ya kuanika ratiba ya maonyesho yao kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka itakayoptangazwa muda wowote kuanzia leo ili mashabiki wao wakae tayari kuwapokea.

Sevilla, Valencia, Juve, Benfica hizoo nusu fainali Europa League

Pirlo kati akipongezwa na wenzake kwa kufunga bao la kuongoza
Sevilla walipokuwa wakiinyoosha Porto
KLABU za Hispania zimeendelea kung'ara Ulaya baada ya jana Valencia na Sevilla kupindua matokeo na kufuzu Nusu Fainali ya Ligi Ndogo ya Ulaya (Europa League) dhidi ya Basel na Porto, huku mabingwa watetezi wa Italia, Juventus nao wakitinga hatua hiyo kwa kuibamiza Olymnpique Lyon.
Valencia iliyokuwa imetandika mabao 3-0 na Basel iliitupa nje timu hiyo ya Uswisi baada ya kuwacharaza mabao 3-0 na kuingi kwenye muda wa nyongeza na kushinda mabao mawili ya ziada na hivyo kufua Nusu Fainali kwa kishindo cha mabao 5-3, huku ndugu zao wa Sevilla waliolala 1-0 katika mechi ya kwanza iliishindilia Porto ya Ureno mabao 4-1 na kufuzu kwa jumla ya mabao 4-2.
Katika mechi ya Juventus iliyoshinda mechi ya ugenini bao 1-0, ilianza kuwashutua wageni wao kwa kuwatangulia kwa bao la mapema la dakika ya nne lililofungwa na Andre Pirlo kabla ya Jimmy  kusawazisha katika dakika ya 18 akimalizia kazi nzuri ya Mvuemba.
Hata hivyo katika dakika ya 68 Samuel Umtiti alijifunga bao katika harakati za kuokoa shambulizi langoni mwake na kuiwezesha Juve kushinda mabao 2-1 na kusonge mbele kwa mabao 3-1.
Katika mechi nyingine ya marudiano ya robo fainali ya michuano hiyo, AZ ya Uholanzi ilishindwa kutamba mbele ya Benfica ya Ureno baada ya kufungwa mabao 2-0 na hivyo kungoka kwa jumla ya mabao 3-0.
Mabao ya wenyeji yalipachikwa wavuni katika kipindi na mshambuliaji wake nyota Rodrigo katika dakika ya 39 na 71 yote yakitokana na pasi za Salvio.
Washindi hao watasubiri kujua wataumana na nani katika droo inayotarajiwa kutolewa leo kama itakavyokuwa kwa ile ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo Hispania imetoa timu mbili Real Madrid na majirani zao Atletico Madrid, watetezi Bayern Munich na Chelsea ya England.