STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 2, 2013

Borussia Dortmund yamtolea macho Podolski

http://img.thesun.co.uk/multimedia/archive/01595/PODOLSKI_1595719a.jpg
Lucas Podolski



KLABU ya Arsenal inakabiliwa na changamoto kubwa ya kumbakisha mshambuliaji wake nyota Lucas Podolski, baada ya mchezaji huyo aliyesaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Ecuador kunyemelewa na wana fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya, Borussia Dortmund.
Podolski, aliyewahi kuripotiwa na gazeti la The Sun mwezi Aprili kuhitajiwa na Atletico Madrid, alitua Emirates mwaka jana kwa kitita cha Pauni Mil. 11, lakini kwa sasa atupiwa macho na Dortmund iwap[o Arsenal inaridhia kumuachia.
Klabu hiyo ya Ujerumani imepata jeuri ya kumtaka Podolski aliyesajiliwa na Arsenal akitokea timu nyingine ya Bundesliga ya Cologne kutokana na kuvuna mamilioni ya fedha kwa kumuuza Mario Gotze kwa kitita cha Pauni Mil. 31.5 na nyota wake mwingine Robert Lewandowski akiwa njiani kumfuata mwenzake kwa mabingwa hao walioweka rekodi msimu huu kutwaa taji la Ligi ya Ulaya, Bundesliga na Kombe la Ujerumani.
Hata hivyo Dortmund itabidi ifanye kazi ya ziada kumshawishi Arsene Wenger kumtoa mchezaji huyo wakati akiwa ameaminiwa na mabosi wake kuendelea kukisuka upya kikosi hicho ili angalau kufuta 'ukame' wa mataji katika klabu hiyo uliodumu kwa miaka kadhaa sasa.
Mshambuliaji huyo mwenye asili ya Poland na aliyeichezea timu ya taifa ya Ujerumani mara 109 na kuifungia mabao 46, tangu alipotua Arsena; ameichezea mechi 33 za Ligi na kuifungia mabao 11 na amekuwa akinukuliwa akifurahia maisha Emirates.

No comments:

Post a Comment