STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 2, 2013

Simba, Yanga kutoshiriki Kagame, kisa....!

 
Simba

Mabingwa watetezi wa Kagame, Yanga
VIONGOZI wa klabu ya soka ya Simba na Yanga wanatarajiwa kukutana haraka iwezekanavyo kwa nia ya kutoa msimamo wao juu ya kwenda Sudan kushiriki michuano ya Kombe la Kagame ambayo inatarajiwa kuanza katikati ya mwezi huu.
Michuano hiyo ilitangazwa na Baraza la Vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati - CECAFA kuwa ingefanyika mjini Darfur -Sudan, lakini serikali ya Tanzania imetoa tamko kuhusu timu za Simba na Yanga kwenda kushiriki michuano hiyo huko Sudan kwenye eneo ambalo limekuwa likiandamwa na vurugu kwa miaka kadhaa sasa.
 Kwa mujibu wa msemaji wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga ni kwamba serikali haidhani ni busara kwa vilabu vya Simba na Yanga kwenda kwenye eneo hilo kushiriki Kagame Cup kutokana hali mbaya ya usalama iliyopo Darfur.
Kamwaga aliadnika hivi katika ukurusa wake wa Facebook;
Breaking News...... Serikali imesema haioni busara ya Kagame Cup kupigwa Darfur.... Hakuna hoteli ya maana na watu wanashauriwa kutembea na fulana zinazozuia risasi kupenya... Nadhani hii ndiyo stori kubwa ya kimichezo kwa leo.... Je, mnadhani itakuwa busara kwa Simba na Yanga kushiriki?
Hata hivyo taarifa zilizopatikana mchana huu ni kwamba viongozi wa Simba na Yanga kwa nafasi zao wanatarajiwa kukutana kujadili tamko hilo na kutoa msimamo wao kama wataenda Sudan au la, kwa hofu ya machafuko yanayoendelea huko.
Kagame ili[elekwa huko kwa nia ya kuhamasisha amani katika mji huo, lakini hali haionyeshi matumaini na wadau wengi wanadhani si busara timu za Tanzania kwenda kwa kuhofia kutokea maafa ywa wachezaji wa timu hizo. TUSUBIRI Tuone

No comments:

Post a Comment