STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 2, 2013

Ruvu Shooting waanza kuimarisha kikosi chake

Kikosi cha Ruvu Shooting Stars

KLABU ya soka ya Ruvu Shooting ya Pwani imemsajili mchezaji Cosmas Ader Lewis kwa mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia klabu hiyo katika Ligi Kuu Tanzania Bara.
Cosmas aliyeichezea kwa mkopo African Lyon msimu uliopita akitokea Azam, alisaini mkataba huo mwishoni mwa wiki kwenye ofisi za klabu hiyo ya jeshi zilizopo Kikosi cha Jeshi 832 Ruvu JKT Mlandizi, Kibaha-Pwani.
Mchezaji huyo alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja na klabu ya Azam ambao umeisha na kuifanya Ruvu kufanikiwa kumnyakua na kuzizidi kete timu nyingine zilizokuwa zikimnyemelea ikiwamo Simba.
Msemaji wa timu hiyo Masau Bwire aliiambia MICHARAZO kuwa usajili wa mchezaji huyo ambaye ni mshambuliaji kinda aliyezaliwa Novemba 1995, una lengo la kuifanya Ruvu Shooting ifanye vyema kwa msimu ujao baada ya msimu uliosha hivi karibuni kushindwa kutimiza malengo yao ya kumaliza kwenye 5 Bora.
Bwire alisema kunyakuliwa kwa mchezaji huyoa ni mwanzo wa timu yao kujiimarisha kwa msimu ujao ambao huenda ukaanzxa kati ya Agosti na Septemba mwaka huu.
"Tunaamini kutua kwa Lewis Ruvu Shooting kutakuwa na tija na ufanisi mkubwa kwa msimu ujao kwani ni mmoja wa wachezaji mahiri na ndiyo maana tumeamua kumnyakua, "alisema Bwire.
Bwire alisema usajili wao kwa kikosi cha msimu ujao ufanywa kwa umakini mkubwa ili kuondoa dhana kwamba timu za majeshi ni wasindikizaji tu katika Ligi Kuu Tanzania Bara, ambayo kwa sasa bingwa wake ni Yanga ambao walinyakua nafasi ya kwanza na kufuatiwa na Azam kisha Simba.

No comments:

Post a Comment