STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 2, 2013

Makocha Ilala wainyuka Kinyerezi Veterani


TIMU ya makocha wa soka wilayani Ilala, Ilala Coaches Fc, imeinyuka Kinyerezi Veterani kwa bao 1-0 katika mfululizo wa mechi zao za kila mwezi, mchezo uliochezwa uwanja wa Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa, Ilala Dar es Salaam.
Bao pekee la makocha hao, lilitumbukizwa kimiani na Hashim Gadiola na kuendeleza ubabe wa kikosi chao kinachojumuisha makocha mbalimbali wa Ilala.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Makocha Ilala, TAFCA-Ilala, Hugho Sseseme Makocha Ilala walionyesha uwezo wa hali ya juu licha ya wapinzani wao kuonyesha upinzani na kusababisha ushindi katika mechi hiyo ya leo kuwa kiduchu.

No comments:

Post a Comment