STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 2, 2013

Stars kujipima nguvu na Sudan kabla ya kesho kwenda Morocco


KIKOSI cha timu ya taifa, Taifa Stars kilichopo kambini mjini Addis Ababa, Ethiopia kujiandaa na mechi ya kuwania tiketi ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco Juni 8, leo itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan.
Stars chini ya Kocha wake, Kim Poulsen, iliyopiga kambi katika Hoteli ya Hilton kujiandaa na mechi hiyo, ipo nafasi ya pili kwenye kundi la C; nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura aliyehojiwa na kituo kimoja cha redio nchini alisema kuwa pambano hilo litatumiwa na kocha Poulsen kukiangalia kikosi chake kabla ya kesho kuondoka kueleka Morocco.
Wambura alisema mara baada ya mechi hiyo wachezaji na viongozi wa Stars watakwenda Ubalozi wa Tanzania nchini humo walikoalikwa na Balozi Joram Biswaro, ambapo watapata fursa ya kukutana na baadhi ya Watanzania wengine waishio nchini huo kwa ajili ya kuwaaga.
Kikosi cha nyota 22 kitaondoka Ethiopia alfajiri ya kesho kwenda Marrakech, Morocco kupitia Cairo, Misri ambao ni Juma Kaseja, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vincent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi.


No comments:

Post a Comment