STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 2, 2013

Mwili wa Ngwair wakwama tena, sasa kutua Jumanne

https://fbcdn-sphotos-e-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/p480x480/579293_526768957387103_1440212486_n.jpg
Ngwair

MWILI wa aliyekuwa nyota wa muziki wa Hip hop nchini, Albert Mangwea 'Ngwair' uliokuwa uwasili nchini huu umeshindikana na sasa utawasili nchini Jumanne ukitokea Afrika Kusini ambapo ndipo msanii huyo alipopatwa na mauti.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Mazishi ya msiba wa msanii huyo, umewaomba radhi Watanzania ambao wamekuwa na shauku ya kuupokea mwili wa kipenzi chao huyo, aliyekuwa ametangazwa awali angetua jana mchana kabla ya kubadilishwa na kuelezwa ungetua leo saa 8 mchana.
Taarifa rasmi ya kamati hiyo inasomeka hapo chini, ingawa taarifa zaidi kutoka Afrika Kusini zinasema kuwa mwili wa Ngwair utawasili nchini Jumanne mchana na kuagwa siku inayofuata kabla ya kwenda kuzikwa Morogoro Alhamisi.
Kwa mujibu wa ujumbe wa mtangazaji wa Clouds Millard Ayo aliyepo Johannesburg, Afrika Kusini aliotwitte kwenye akaunti yake ni kwamba mwili wa Ngwair utawasilia Jumanne mchana.

                  TAARIFA YA KAMATI NDIYO HII HAPA:
Kamati ya msiba tunaomba kutoa ya taarifa kwamba mwili wa Ndugu yetu Albert Mangwea hautoweza kufika siku ya jumapili ya tarehe 2/06/2013 kama ilivyo taarifa hapo awali, hii ni kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu.Kwa sasa tunasubiri taarifa kamili kutoka kwa wenzetu/wawakilishi wetu waliopo nchini Afrika Kusini, mara tutakapopata taarifa hizo tutawafahamisha zaidi.Tunaomba radhi watanzania wote kwa usumbufu wote uliojitokeza tushirikiane na uvumilivu kwa hili.
Asante
Mwenyekiti wa Kamati
Kenneth Mangweha
…………………………………
Msemaji wa Kamati
Adam Juma
……………………….

No comments:

Post a Comment