STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 2, 2013

Mwanamke aishi kama mkimbizi baada ya kunusurika kuchinjwa


Mary Mbosa aliyenusurukia kuchinjwa na mtalaka wake na kulzaimika kuishi porini kama mkimbizi.

Na Gustav Chahe, Iringa



MAMA mmoja mkazi wa Itunundu – Pawaga katika Mkoa wa Iringa Mery Mbosa anaishi kama digidigi baada ya kunusurika mara kadhaa kuchinjwa na mtalaka wake na kulazimika kuhama kijiji kwa ajili ya kunusuru maisha.



Akiongea na mtandao huu jana, Bi Mbosa alisema maisha yake yapo hatarini kutokana na kuvamiwa na mtalaka wake mara kadhaa akiwa nyumbani na kumuumiza.



Alisema alilazimika kutalakiana baada ya mwanamume huyo kuwa mkorofi kiasi cha kupigwa, kutokuwa huru kutumia mazao ambayo walilima wote na hata kutokuwa huru kuongea na watu hata kama ni ndugu zake kwa madai kuwa ni wivu wa kimapenzi.



Alisema mtalaka wake amegeuka kuwa mnyama na kufika nyumbani kwake usiku wa manane na pindi anapokuta mlango umefungwa huanza kurusha mawe madirishani huku akitaka kuvunja mlango ili kuingia kumdhuru.



Amemtaja mtalaka wake kuwa ni Phabiani Msilamgunda ambaye miezi ya hivi karibuni alikutana na ye njiani akielekea shambani akamvamia akiwa na kisu kwa kutaka kumchinja na kuokolewa na watu ambao walikuwa jirani.



“Ilikuwa 23 Machi mwaka huu nilikuwa nikielekea shambani nikakutana na mtalaka wangu akiwa na kisu mkononi akanivamia huku akisema nakuchinja laeo lakini kwa bahati nzuri kulikuwa na watu jirani wakaniokoa vinginevyo ningekuwa marehemu.



“Lakini hata hivyo amekuwa akimtukana hata mama yangu mzazi (mama mkwe) akitaka kupiga pia na kila wakati nimekuwa nikishtaki hadi ofisi zinanichoka pamoja na kuwa ninapokelewa na akiitwa haendi kwa sababu amekuwa mbabe” alisema bi Mbosa.



Hata hivyo Mbosa alisema kuwa aliwahi kupigwa na kuumizwa vibaya na kulazimika kushtaki mahakamani japo kuwa hukumu ilivyotolewa haikuwa ya haki na kuhatarisha zaidi maisha yake.



“Nilipigwa na kuumizwa vibaya kesi ikapelekwa mahakamani lakini hukumu ilivyotolewa haikuwa ya haki kwangu na baada ya hukumu maisha yangu yamekuwa ni ya hatari zaidi” alisema.



Kwa mujibu wa maelezo ya wananchi wa kijiji hicho ambao wameeleza kushuhudia mama huyo akinusurika kuuawa na jinsi maisha yake yanavyozidi kuwa mabaya, walisema kiburi cha Msilamgunda kinatokana na dada yake ambaye ni diwani wa viti maalum (CCM).



Gazeti hili limebaini kesi ambayo mama huyo hajaridhika na hukumu ni Jinai No. 22/2013, mshitakiwa Phabiani Msilamgunda ambayo ilitolewa hukumu Mei 21 Mwaka huu.



Imeelezwa kuwa katika utoaji huku hiyo hakimu aliyetajwa kwa jina moja la Masuwe alimtaka mtuhumiwa alipoe faini ya shilingi laki mbili pamoja na gharama ya kesi shilingi 45 elfu jambo ambalo lilifanyika hivyo na mtuhuhumiwa kuwa huru kwa vitisho kuwa lazima ammalize mwanamke huyo.



Pamoja na kutokuridhika na hukumu iliyotolewa, Mkuu wa kituo cha Polisi cha Pawaga Fedrick Nyavilwe anatuhumiwa kumdhurumu mama huyo na kuiomba serikali kumsaidia ili aishi kama wanavyoishi wananchi wengine.



Nyavilwe anatuhumiwa kumdhurumu mwanamke huyo mbegu ya mpunga na kumfanya kuwa mtumwa kwa kukosa chakula bila kujua hatima ya maisha yake.



“Baada ya hukumu nilikwenda shambani nilikokuwa ninaanda mbegu ya mpunga kwa ajili ya kupanda nikakuta watu wananing’oa, nilipouliza walisema wametumwa na Mkuu wa kituo cha polisi. Hivi sasa naishi kama ndege jamani sijui nitakula nini kwa sababu hata mashamba niliyokuwa nalima nilinyang’anywa na mbegu niliyokuwa nimeandaa kwa ajili ya kupanda polisi wameninyang’anya” alisema.



Alipotafutwa kwa njia ya simu kwa ajili ya kutolea maelezo, Veronica Msilamgunda ambaye ni ndugu na Phabian Msilamgunda alisema hawezi kuzungumza chochote kwa kuwa yupo kwenye mkutano.



Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho Joseph Malinga alipotafutwa kwa ajili ya ufafanuzi Alikiri kuwa mama huyo ni mhanga mkubwa na anaishi kama mkimbizi kwa hofu ya kuuawa.



“Nalijua sana hilo na ninashukuru kwa kuwa umenitafuta ili nikueleze. Maisha ya huyo mama hatuji yataishia wapi kwa sababu hali ilivyo kwa sasa ni ngumu na anaishi kama mkimbizi.




“Hata akiwa sehemu yenye ulinzi anaona kama hakuna ulinzi kwa sababu ya kile anchofanyiwa. Kiujumla hata sisi viongozi wa kijiji tunaishi kwa mashaka kwa sababu tunatishiwa kuuawa tunapotaka kutafutas suluhu ya huyo mama. Huyu mwanaume tunashindwea kuelewa kama ni mtu wa kawaida maana amegeuka kuwa kamas samba” alismea Malinga.



Hata hivyo alisema anaomba kwa watu wanaoweza kumsaidia mama huyo kupata hifadhi ili aondokane na maisha ya kuishi kama digidigi kule kijijini.

No comments:

Post a Comment