STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 16, 2013

MIUJIZA! Mtoto azaliwa na Tasibhi shingoni mwake

clip_image001KATIKA tukio la kustaajabisha, mtoto mmoja huko nchini Nigeria amezaliwa akiwa na tasbihi shingoni mwake na kuwashangaza wengi akiwemo wakunga waliomzalisha mama wa mtoto huyo.
Maelfu ya watu walifika hospitali binafsi ya uzazi kwenye jiji la Kotaworo eneo la Bida, iliyopo jimbo la Niger  Jumapili, kwa lengo la kwenda kumshuhudia mtoto wa kike aliyezaliwa akiwa amevaa Tasbihi inayotumika katika utajo wa Mwenyezi Mungu shingoni mwake.
Inaelezwa kwamba mama wa mtoto huyo ambaye ana miaka ya kati, Adijat, alikimbizwa hospitali karibu na nyumbani kwa  Mohammed Bello Masaba, mida wa saa 8 mchana na baada ya pilika za uzazi alifanikiwa kujifungua mtoto huyo.
Kwa mujibu wa mmiliki wa hospitali hiyo ya uzazi, Alhaji Abubakar Baiwa Shasha ambaye ndiye aliyesimamia zoezi hilo la kujifungua alisema; 
“Nilishtuka nilipoona mtoto anatoka akiwa na Tasbihi shingoni mwake, na wakati wa uzazi mtoto alizaliwa tasbihi hiyo ilikuwa nyeusi," alisema Shasha.
“Ila nilishangaa baada ya muda tasbihi hiyo ilibadilika na kuwa nyeupe huku kukiwa na watu wengine wamezunguka.”
“Mara baada ya habari hiyo kusambaa mjini, maelfu ya watu walifika kwenye hospitali hiyo ya uzazi huku wakisema “Allahu Akibar; Allahu Akibar (Mungu ni Mkubwa) huku wakifika na kumgusa mtoto huyo.”
Juhudi za kumpata Baba wa mtoto huyo aitwaye Isah, ambaye anatokea eneo la Loma ndani ya Jimbo la Kwara  zilishindikana baada ya kukataa kuongea na mtoa habari.
Mwanachuo mmoja wa Kiislamu, Malam Idiris Ndajiwo alisema, kuzaliwa kwa mtoto huyo akiwa na kitu kama hicho inaonyesha ukuu wa Allah (SW). Kuzaliwa kwa mtoto huyu leo, kwenye mji huu na eneo hili (Kutaworo) ni kitu kikubwa kwa Waislamu. Hii hakika inakuja kuonyesha kwamba Allah ndiye mwenye kupanga kwa lolote kutokea kwa yeyote kwenye ulimwengu huu.”

No comments:

Post a Comment