STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 16, 2013

Pigo! Jaji Chipeta afariki dunia




Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Buxton Chipeta enzi za uhai wake
HABARI zilizopatikana hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania,Buxton Chipeta amefariki dunia muda mfupi uliopita.

Kwa mujibu wa mmoja wa wanafamilia, Jaji Chipeta alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kisukari ambapo ilifikia wakati akalazimika kukatwa vidole kadhaa vya miguuni.

Enzi za uhai wake, Jaji Chipeta aliweza kujijengea heshima katika kazi yake na kufikia kuwa mmoja wa majaji wanaoheshimika mno hapa nchini.
 

Pia Jaji Chipeta aliwahi kuwa miongoni mwa majaji wa Tume ya kurekebisha Sheria yeye akiongoza kanda ya Dar es Salaam.
 

MICHARAZO  inaungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi ya kuondokewa na mpendwa wao na kuwaombea kwa Allah Subhana Wataala kuwa na subira na uvumilivu kwa kuamini kuwa kila nafsi itaonja mauti na kurejea kwa aliyetuumba. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema.

No comments:

Post a Comment