STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 16, 2013

Waliokufa Darfur waagwa, JWTZ lakana ongezeko la vifo



WAKATI miili ya wanajeshi saba wa Tanzania waliouwawa huko Darfur, Sudan wakiagwa kwa heshima nchini humo na kuanza mipango ya kurejeshwa nchini kwa ajili ya mazishji yake, Jeshi la Watanzania Tanzania, JWTZ, limekanusha taarifa za kuwepo kwa ongezeko la vifo vya askari wake.
Msemaji wa jeshi hilo. amenukuliwa hivi punde na Clouds FM kwamba hakuna askari mwingine aliyefariki japo alikiri mmoja wa majeruhi wa tukio hilo hali yake ni tete kiasi cha kuhamishwa hospitali aliyokuwa akipewa huduma na wenzake 9 na kupelekwa Khartoum kwa matibabu zaidi.
"Hatujui hizi taarifa zinazowekwa kwenye mitandao ya kijamii wanazipata wapi wakati sisi ndiyo wenye kuhusika na tukio, ila ukweli ni kwamba hakuna idadai iliyoongezeka ya vifo na jeshi halina sababu ya kuficha kitu," alisema Kanali Kapambala Mgawe Msemaji wa JWTZ.
Kanali Mgawe alisema hali za majeruhi wengine tisa zinaendelea vyema kiasi cha kuweza kutembea wenyewe japo mwenzao mmoja amehamishiwa Khartoum kwa matibabu zaidi na kuwataka watanzania wasiwe na hofu wala kuziamini taarifa hizo zinazoandikwa na kuwekwa kila muda katika mitandao hiyo.
"Watanzania hawana haja ya kuwa na hofu hali za askari wetu zinaendelea vyema japo mmoja hali yake siyo nzuri sana na kulazimika kuhamishiwa mjini Khartoum kwa matibabu zaidi na wenzake tisa tunashukuru kwani wanaendelea vyema," alisema.
Hapo chini ni baadhi ya picha za miili ya wanajeshi hao ikitolewa heshima na wanajeshi wenzao, sambamba na majeruhi waliolazwa baada ya tukio hilo la kushambuliwa na waasi wakati katika msafara wao wa kulinda amani katika jimbo hilo la Darfur.


The African Union – United Nations Mission in Darfur (UNAMID), held a memorial ceremony, in Nyala, the capital of South Darfur, to honor the seven fallen peacekeepers who lost their lives in the 13 July attack in South Darfur. The bodies are scheduled to be repatriated to Tanzania, the home country of the fallen peacekeepers. In addition to the seven killed, 17 military and police personnel were wounded, among them two female Police Advisors, all of whom are recovering from their injuries in UNAMID’s hospital in Nyala, South Darfur. Photo by Saidi Msonda, UNAMID.












 On 14 July 2013, following a 13 July attack in which seven military peacekeepers of the African Union - United Nations Mission in Darfur (UNAMID) were killed and 17 military and Police personnel wounded, among them two female Police Advisers, Joint Special Representative Mohamed Ibn Chambas visited the wounded peacekeepers at UNAMID’s hospital in Nyala to provide encouragement and support. Photos by Albert González Farran, UNAMID.


No comments:

Post a Comment