STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Jaji Mutungi ndiye Msajili wa Vyama vya Siasa, amrithi Tendwa


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTYy1tXHsu-VoVz-W0VGnrZjYG-Y5qEX-6aQrlO10GYaiMhcTSpZ30Oe6u4ZyMpbbDQgI8NMkE1GvZUTDWZDzL25fWf8J5rtoRZZFvxl45rBygkFyi4BKfKnt4iiunig1ffG3qZcidwxa2/s640/P+1.jpg
Jaji Francis Mutungi (kulia) alipokuwa akiapishwa na Rais JK mara alipoteuliwa Jaji wa Mahakama Kuu Juni mwaka jana.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amemteua Jaji Francis S.K. Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam leo Jumatatu (Agosti 5, 2013 na kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita (Agosti 2, 2013).
Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama na Siasa, Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu utumizi wa umaa kwa mujibu wa sheria.
Kabla ya uteuzi huo Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma.

No comments:

Post a Comment