STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Huyu ndiye 'Tanzania One' Juma Kaseja

Kipa Juma Kaseja akiwa na Katibu wa kituo cha yatima cha New Life Orphans Home Hamad Kombo walipokitembelea kituo hicho jana ambapo watoto walipagawa naye wakionyesha wanaomfuatilia kupita maelezo.

Ebu niambie wewe msimu huu unaenda wapi? Ashanti au Fc Lupopo? Kaseja akiteta jambo na Mlezi wa klabu ya Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' huku wachezaji wenzake wakisikiliza kwa makini na watoto wakiwa bado wana hamu ya kufurahia naye kama wanvyoonekana kando yake kwa ndani..

Huyo hana lolote anaenda zake Mbeya City? Kaseja akiteta na beki wa zamani wa Yanga na Reli, Yahya Issa huku Ticotico na Faraji wakisikiliza.
Kaseja mkekani na watoto
Akimakinika na watoto ambao baadhi walikuwa wakimshangaa


Kwani hiyo simu inauzwa kiasi gani? Ni kama dogo huyo anamuuliza Kaseja
Watoto wakiwa sambamba na Kaseja

Kaseja akizungumza na watoto waliotaka kupiga naye picha jana kwenye kituo cha kulelea yatima cha New Life Orphans Home
Yaani kila mtoto alitaka kuwa karibu na Kaseja

Kaseja na mlezi wa Golden Bush, Onesmo 'Waziri Ticotico' aliyembeba mtoto katikapicha ya pamoja na watoto.
 
Sheikh huwezi kutoka bila kupiga picha na miye! Katibu wa kituo cha kulelea yatima, Hamad Kombo(kati) akiwa pichani na Kaseja (kushoto)
HUENDA kipa Juma Kaseja ndiye mchezaji anayetambuliwa na kufahamika kirahisi nchini iwe kwa watoto ama hata wanawake ambao mara nyingi huwa siyo wafuatiliaji wa soka.
Mara kadhaa katia mahojiano yangu na wasanii au wanamichezo hasa wa kike wanaoshabikia soka wengi humtaja Kaseja kama mchezaji wanayemjua kwa umahiri wake, wengine huwa ni Mrisho Ngassa, Ally Mustafa 'Barthez', Athuman Idd 'Chuji' na wakati mwingine Emmanuel Okwi japo kwa sasa hayupo nchini.
Kitu gani kinachomfanya Kaseja awe kivutio na gumzo midomoni mwa watu, kama ambavyo ilivyo sasa baada ya kutemwa na Simba? Sina shaka ni umahiri wake dimbani, nidhamu na kule kujiweka chini licha ya usupa staa alionao.
Jana wakati timu ya Golden Bush FC ilipowatembelea yatima wa kituo cha New Life Orphans Home, Kaseja ndiye aliyekuwa gumzo kwa watoto na hata uongozi wa kituo hicho na kuomba kupiga naye picha, huku kipa wa Mbeya City, Aman Simba akifananishwa na Chuji kwa mzuzu aliokuwa nao.
Hata wakati wenzake wakiwa wamekaa kwenye mabenchi na viti, Kaseja alijichanganya na watoto katika mkeka kabla ya baadaye wachezaji wenzake wakati wa kupiga picha ya pamoja na watoto kuungana naye kwenye mkeka.

No comments:

Post a Comment