STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Sheria bila Sera 'miyeyusho' mitupu kwa maendeleo ya jamii


Na Suleiman Msuya
KITENDO cha kuwepo kwa sheria bila sera kimetajwa kama moja ya chanzo cha kukwamisha na kudididimiza jitihada za kuleta maendeleo kwenye jamii hapa nchini.
Hayo yamebainishwa na Dk. Frateline Kashaga wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Alisema kumekuwepo kwa utaratibu wa kuwepo kwa sheria bila sera jambo ambalo ukiliangalia kiundani ndicho chanzo kikubwa kinachokwamisha juhudi za kupigania maendeleo hapa nchini kwa utekelezaji haupo.
Dk. Kashaga ambaye pia ni Mwahadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu Cha  Dar es Salaam tawi la (DUCE) alisema ni vema amichakato hiyo ikaenda kwa pamoja ili iweze kuleta tija kwa Taifa.
“Nimekuwa nikifuatilia mara kwa mara sheria zetu ambazo zinaundwa nimegundua mapungufu mengi ambapo kubwa zaidi ni ukosefu wa sera kwa wakati huku sheria ikiwepo kwa muda mrefu jambo ambalo linanishangaza,” alisema.
Mwahadhiri huyo Mwandamizi alisema huu ni wakati muafaka kwa jamii ya wanataaluma kutafakari kwa kina juu ya changamoto hiyo na kuja na mapendekezo ambayo yatakuwa na manufaa kwa nchi.
Alisema ni muhimu kwa Taifa likahakikisha kuwa kunakuwepo kwa sera sahihi ambazo zitafaidisha jamii kwani kutokana na takwimu kunaonyesha nchi zilizoendfelea ndizo zinafaidika kwa rasilimali za nchi.
Dk. Alisema zaidi ya dola bilioni 150 zinapotea kutoka bara la Afrika takribani kila mwaka katika mazingira ambayo hayakubaliki hali ambayo inaonyesha dhahiri kuwa ni ukosefu wa sera sahihi za kusimamia rasilimali za nchi.
Kashaga alisema ni vema Tanzania na Afrika kwa ujumla wakatengeneza sera za kimkakati ambazo zitaweza kufanya mataifa yao kufaidika na rasilimali zilizopo kwa kipindi kirefu.
Aidha mmoja wa changiaji aliweka bayana kuwa uvutiaji wa wawekezaji katika bara la Afrika takwimu zinaonyesha kuwa bara la Afrika linaingiza dola bilioni 130 kwa mwaka kutoka nje ambapo lenyewe linapeleka zaidi ya dola trilioni mbili uwioano ambao sio sahihi.

No comments:

Post a Comment