STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Makamba awataka vijana kuwania nafasi za uongozi


Mhe. January Makamba

Na Suleiman Msuya
MLEZI wa Shirikisho la Vijana wa Vyuo Vikuu wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia January Makamba amewataka vijana nchini kujitokeza na kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia ngazi za mitaa hadi Taifa.
Makamba aliyasema hayo Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu katika kongamano la kujadili rasimu ya Katiba ambayo kwa sasa ipo kwenye mchakato wa mabaraza.
Alisema vijina wanapaswa kutambua kuwa ufumbuzi wa mahitaji yao yao ni pamoja na wao kushiriki moja kwa moja katika kugombea nafasi za uongozi ambazo zinapatikana na kuacha tabia ya kulalamika.
Naibu Waziri alisema ili Taifa liweze kupiga hatua ni dhahiri kuwa mchango wa vijana hasa wasomi unahitajika kwani ndio chachu ya kuleta maendeleo katika nchi na wananchi kwa ujumla.
“Kimsingi vijana wa Tanzania wamekuwa walalamikaji bila kuwajibika ila napenda kuwapa usia huu kuwa njia ya kukomboa Taifa ni sisi kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi na kiutumishi ili tuwe sehemu ya maendeleo,” alisema.
Mlezi huyo alitolea mfano wa Nabii Musa wakati alipoulizwa na Mungu mkononi ameshikilia nini ambapo alimjibu fimbo na kumtaka aiweke chini fimbo hiyo ambayo ilibadilika kuwa nyoka na baadae ilibadilika kuwa fimbo tenda hivyo taaluma zao ziwe ni fimbo kwa kusaidia maendeleo ya Taifa.
Alisema fursa zilizopo nchini zinahitaji vijana kushiriki kikamilifu ili ziweze kuwa na tija kwani kuendelea kusubiri kutachangia nchi kupoteza rasilimali nyingi ambazo zipo.
Naibu Waziri alisema iwapo vijana watakuwa washiriki katika uongozi ni dhahiri kuwa viongozi sahihi wenye uzalendo na uadilifu wanaweza kupatikana bila kuwepo kwa lawama za ufisadi na kashfa nyingine nyingi ambazo zimekuwa zikiibuliwa.
Akizungumzia juu ya kongamano hilo alisema CCM imejipanga kikamilifu ili kuhakikisha kuwa vijana wanashiriki katika majadiliano yoyote ambayo yanahusu Taifa kwa lengo kuu kwamba wao ndio wasimamizi wa rasilimali za nchi.
Makamba alisema vijana wanapaswa kutumia fursa hiyo kuwasilisha hoja ambazo zitasaidia nchi na kuachana na tabia ya kulalamika mara kwa mara bila kuja na suluhisho

No comments:

Post a Comment