STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Mjumbe CCM, awapasha wajumbe Tume ya Katiba

Mjumbe wa CCM, Evod Mmanda
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (MNEC) Evod Mmanda amewataka Wajumbe wa Tume ya Katiba kuacha kufanya kazi ya kujibu mapungufu yaliyopo katika rasimu hiyo kwani huu ni wakati wa Mabaraza kufanya kazi ya kurekebisha na kupendekeza.
Mmanda alitoa kauli hii wakati akiongea na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam ambapo alisema ameshuhudia baadhi ya wajumbe wa Tume wakitoa maelekezo kwa wajumbe wa mabaraza jinsi ya kutoa maoni.
Alisema ni vema Tume hiyo ikatambua kuwa wakati wao wa kuandaa rasimu umepita na sasa ni wakati wa kuyapa fursa mabaraza kutokana sheria inavyotaka jambo ambalo ni muhimu kuheshimiwa.
Mjumbe huyo wa Mkuatano Mkuu alisema CCM wanaamini kuwa fursa zikipatikana upo uwezekano wa kupatikana na kwa katiba ambayo itakuwa na maslahi na Taifa hivyo kuingilia maoni ya watu ni kinyume na katiba inavyotaka.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaasa wajumbe wa Tume ya Katiba kuwa wakati huu ni wakuwaachia wajumbe wa mabaraza kutoa maoni na mapendekezo yao hivyo kukaa na kujibu hoja hizo wakati wanatakiwa kusubiri ni kwenda kinyume na sheria inayowaongoza,: “ alisema.
Mmanda alisema iwapo wajumbe watatumia nafasi elekezi kuwashawishi wajumbe wa mabaraza kukubaliana na mapendekezo yao ni dhahiri kuwa kutakuwepo na katiba ambayo ina mitazamo ya watu wachache.
Alisema kuna mapungufu mengi ambayo yameonekana katika rasimu hiyo hivyo ni wakati muafaka kwa jamii na vijana kwa ujumla kutumi nafasi zao kutoa maoni ambayo yataweza kusaidia kizazi cha leo na kijacho.
Mjumbe huyo ambaye alionyesha dhahiri kutokuunga mkono wa uwepo wa Serikali tatu aliishutumu tume kwa kuweka maoni hayo kwa kile alichodai kuwa haikuwa sehemu ya muuongozo wao kufanya.
Aliweka bayana kuwa yeye ni muumini mkuwa wa serikali mbili hivyo hakuona sababu ya kuwepo mapendekezo juu ya aina ya muungano na kuwataka wachangiaji kupitia nafasi mbalimbali kuwa makini kwa maslahi ya Taifa.
Mmanda alitoa rai kwa vijana wa CCM kuwa watumie nafasi yao kuhakikisha kuwa katiba ijayo inakuwa na maboresho yesnye tija na kuacha tabia ya kuwa katika mitazamo ya watu amabao wanaweza kuwa na maslahi yakiuongozi.

No comments:

Post a Comment