STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Kazimoto aomba radhi Watz, Simba kuvuna Mil. 62

Mwinyi Kazimoto

KLABU ya Al-Makhia ya nchini Qatar, imekubali kutoa kiasi cha Dola la Kimarekani 40,000 ambazo ni zaidi ya Sh milioni 62 za Tanzania ili kukamilisha usajili wa kiungo Mwinyi Kazimoto, aliyetokea Simba ya Dar es Salaam.


Balozi wa klabu hiyo kwa Tanzania, Boniface Pawasa, alisema kuwa klabu yake imekubali kutoa kiasi hicho cha fedha ili kukamilisha usajili wa Kazimoto ambapo katika mkataba wa makubaliano baina ya Simba na klabu hiyo, Wekundu wa Msimbazi watakuwa wakipata asilmia 20 ya mapato kila mchezaji huyo atakapokuwa anauzwa.

“Tumefanikiwa kukamilisha baadhi ya mambo ya msingi ambayo yanamhusu mchezaji mwenyewe, lakini pia klabu ya Simba ambayo ndiyo wanaommiliki.
“Tunaelewa kuwa aliondoka katika mazingira yasiyokuwa bora kwa sababu kulikuwa  na majukumu ya kitaifa, lakini klabu yake haikuwa imeridhia lakini amewaomba radhi wadau wote waliokwazwa na  hali hiyo,” alisema Pawasa, nyota wa zamani wa Simba ambaye pia alishaitumikia Al-Makhia  inayoshiriki Ligi Daraja la kwanza nchini humo.

Mbali na kitita hicho, lakini kwa upande wa maslahi atakuwa akipokea mshahara wa Sh milioni 15 kwa mwezi pamoja na marupurupu mengine ya msingi ambayo yataendelea kuinua kipato chake.
Kwa upande wake, Kazimoto aliliambia Dimba kwamba kitendo alichofanya si kizuri na anakiri kosa, hivyo anawaomba radhi Watanzania wamsamehe na kwamba atakuwa balozi mzuri kwa nchi yake.

“Ni kweli nilifanya makosa, lakini naomba Watanzania wanisamehe kwa kile kilichotokea, ila ilikuwa kwenye harakati za kutafuta maisha tu,” alisema Kazimoto kupitia mtadao wa kijamii wa Facebook.

Mwinyi Kazimoto alisajiliwa na Simba katika usajili wa mwaka 2011 akitokea JKT Ruvu Stars ya mkoani Pwani, ambapo sasa kazi iliyobakia ni Simba kutoa ruhusa kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) hufanya uhamisho wa kimatifa ambao utaombwa na chama cha soka cha Qatar (QFA).

Lenzi ya Michezo

No comments:

Post a Comment