STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Tumba Swedi 'Mdudu Kiwi' atua Ashanti United

Tumba Swedi 'MduduKiwi' (kulia) akiwa na Jackson Chove 'Mandanda' walipokuwa Moro United


BEKI wa zamani wa Azam na Moro United, Tumba Swedi aliyekuwa China akijaribu kusaka nafasi ya kucheza soka la kulipwa nchini humo, amerejea na kutua Ashanti United kwa ajili ya kuichezea katika Ligi kuu Tanzania Bara inayoanza Agosti 24.
Akizungumza na MICHARAZO kutoka Kigoma ilipo kambi ya Ashanti, Swedi alisema kuwa mipango yake ya kucheza China imeshindikana na wiki mbili zilizopita amerejea nchini na kuingia mkataba wa miaka miwili na Ashanti iliyorejea tena katika Ligi Kuu.
Beki huyo wa kati mwenye uhusiano na nyota wa zamani wa Simba na Yanga, Said Swedi 'Pannuci' na Salum Swedi 'Kussi' anayeichezea Mtibwa Sugar, alisema anachofurahia ni kwamba Ashanti imekubaliana naye aichezea na ikitokea nafasi ya kuondoka haitakuwa na kikwazo kwake.
"Ingawa nimerejea, lakini kuna mchakato naendelea kuufanya ambapo kama utakaa vyema huenda Septemba nikatimka tena nje ya nchi, ila Ashanti nimewafahamisha na kukubaliana nami ndiyo maana nimesaini mkataba huo wa kuitumikia wakati nikiwa bado nipo nipo Bongo," alisema.
Mchezaji huyo anayemudu pia kiungo namba sita na kucheza kama mshambuliaji wa kati, alisema hakuona sababu ya kukaa tu bila kujiunga na timu yoyote kama alivyofanya msimu uliopita tangu Moro United ilipoteremka daraja.
Swedi aliyeanzia soka lake katika klabu ya Friends Rangers inayocheza Ligi Daraja la Kwanza kabla ya kuwa miongoni mwa walioiwezesha Kinondoni kutwaa ubingwa wa Copa Coca Cola 2007 na kusajiliwa timu ya vijana na Azam kabla ya kupandishwa timu ya wakubwa, alisema kiu yake kucheza soka la kulipwa barani Ulaya, lakini atatafuta uzoefu kwanza barani Asia.

No comments:

Post a Comment