STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 5, 2013

Umeme Majanga! Mabwawa yote ya kuzalisha umeme yakauka

Prof.  Muhongo
Na Suleiman Msuya
WAZIRI wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amesema takwimu zinonyesha kuwa kwa sasa hamna bwawa lolote la maji ya kuzalisha umeme ambalo lenye maji ya kutosha ya kuzalisha umeme wa kutosha hapa nchini.
Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam wakati akijibu swali la mwandishi habari hii aliyetaka kujua ni kwanini Serikali haikutaka kutumia Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) ili kuzalisha umeme pamoja na kwamba tafiti zinaonyesha kuwa lingeweza kuzalisha umeme wa zaidi ya megawati 3500 iwapo kungekuwepo na uwekezaji.
Profesa Muhongo alisema upo uwezekano wa tafiti kuonyesha hivyo ila kwa sasa serikali ipo katika harakati za kuleta umeme ambao utaweza kumfikia kila Mtanzania kwa gharama ndogo bila tatizo lolote.
Alisema serikali iliwataka RUBADA kutoa taarifa za uhakika kuhusu uwepo wa maji ya uhakika ambayo hayataweza kupungu jambo ambalo halijafanyika hadi sasa hivyo wao kama wasimamia sera mikakati yao ni kuhakikisha kuwa wanatatua matatizo makubwa ya umeme yaliyopo.
“Mimi kila siku napokea taarifa kutoka kwa wasaidizi wangu na wanasema hakuna bwawa hata moja ambalo lina maji ya kutosha ya kuzalisha umeme hivyo kwa sasa ni vema jamii ikajua kuwa sisi tunajikita katika vyanzo ambavyo havina changamoto,” alisema.
Waziri huyo alisema wao kama serikali wamejikita katika uwekezaji wa uzalishaji wa umeme wa gesi, jua, makaa ya mawe na vyanzo vingine ambavyo ni vizuri na rahisi katika uzalishaji wa umeme.
Alisema iwapo mvua zitanyesha wanaweza kufikiria vyanzo hivyo kama njia ya kutatua tatizo ila kwa sasa macho na nguvu zao zipo katika vyanzo hivyo ambavyo amevitaja kwani havina gharama kubwa ya uzalishaji.
Profesa Muhongo alisema mikakati ya Serikali ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2015 kunakuwepo zaidi ya uniti 2000 za umeme ambazo zinazalishwa hapa nchini hali ambayo itachangia kukuza uchumi.
Aidha akizungumzia maamuzi ya kuleta gesi mkoani Dar es Salaam kutoka mtwara alisema hilo ni jambo ambalo halina mjadala kwani Dar es Salaam ndipo mahali penye chanagamoto nyingi za umeme pamoja na uzalishaji mkubwa wa bidhaa mbalimbali.
Muhongo alisema suala la kwanini usambazaji usianze katika mikoa ambayo bado haijapata huduma ya umeme wa uhakika alibainisha kuwa lengo la Serikali ni kufikisha huduma hiyo kwa jamii yote bila ubaguzi ila kwa sasa watafikisha Dar es Salaam na maeneo mengine yatafuata.

No comments:

Post a Comment