STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 24, 2014

Atletico Madrid yafumuliwa ugenini

 Osasuna celebrate
KLABU ya Atletico Madrid usiku wa kuamkia leo imeangukia pua baada ya kupokea kipigo cha mabao 3-0 ugenini dhidi ya Osasuna na kushindwa kuiengua Barcelona ambao walipoteza mechi yao juzi katika Ligi Kuu ya Hispania.
Kipigo cha timu hizo mbili zimeifanya Real Madrid kupumua kileleni, ikiwa na piinti 63, huku Barcelona na Atletico zikisaliwa na pointi zao 60 kila mmoja baada ya kucheza mechi 25 kila mmoja.
Mabao yaliyoinyong'onyesha Atletico ugenini yalifungwa naCejudo katika dakika ya 6 kabla ua Armenteros kufunga la pili dakika ya 21 na kisha Robert Torres kumalizia kazi dakika tatu kabla ya mapumziko.
Katika mechi nyingine, Rayo Vallecano iliifumuliwa nyumbani na Sevilla kwa bao 1-0, Real Betsi kulala pia nyumbani Athletic Club  na Valencia kutakata kwao kwa kuilaza Granada kwa mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment