STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 24, 2014

Carlos Tevez aibeba Juventus nchini Italia

Juventus striker Carlos Tevez
NYOTA wa zamani wa Manchester United na Manchester City, Carlos Teves ameendelea kuonyesha makali yake nchini Italia baada ya jana usiku kuisaidia timu yake ya Juventus kupata ushindi kiduchu wa bao 1-0 na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa Seria A nchini Italia.
Tevez aliifungia Juve bao pekee katika katika pambano lao dhidi ya Torino lililochezwa kwenye uwanja wao wa nyumbani mjini Torino na kuwazima wapinzani wao wa mji huo na kuzoa pointi tatu.
Muargentina huyo alifunga bao hilo lililokuwa la 14 msimu huu katika dakika ya 30 akimalizia kazi ya Kwadwo Asamoah na kuifanya Juve kufikisha jumla ya pointi 66 ikiiwaacha wanaowafukia Roma walioshinda ugenini juzi kwa pointi 9.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana, Lazio ilipata ushindi wa mabao 3-2 nyumbani dhidi ya Sassuolo na leo ligi hiyo itaendelea kwa mechi mbili zitakazowakutanisha OParma dhidi ya Fiorentina na Napoli kuvaana na Genoa.






















No comments:

Post a Comment