STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Abdallah Juma alia na Yondani, refa red card aliyolimwa Jamhuri

Abdallah Juma enzi akiichezea Simba
MSHAMBULIAJI wa Mtibwa Sugar, Abdalla Juma amelia na mwamuzi Zakaria Jacob na beki wa kati ya Yanga, Kelvin Yondani kutokana na kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo wao na Yanga wikiendi iliyopita ulioisha kwa suluhu.
Juma, alisema alilazimika 'kuchapa' Yondani baada ya kushindwa kuvumilia vitendo alivyokuwa akifanyiwa na beki huyo uwanjani alivyovilalamikia kwa refa, lakini alipuuzwa mpaka alipandwa na hasira na kulimwa kadi hiyo.
Mshambuliaji huyo, mmoja wa wachezaji watatu waliofunga hat trick kwenye Ligi Kuu ya msimu huu, alisema Yondani alikuwa akimchezea kibabe wakati mwingine kumfinya, kumpiga makusudi na hata alipolalamika alipuuzwa.
"Laiti mwamuzi angekuwa 'fair' na kusikiliza malalamiko yangu juu ya uhuni nilikuwa nafanyiwa na Yondani naamini nisingefia pale, sijawahi kupewa kadi ya njano wala nyekundu kabla ya tukio hilo la Jamhuri, nimeumia sana," alisema.
Hata hivyo aliwaomba radhi wachezaji wenzake wa Mtibwa kwa kadi hiyo na kuelezwa ni vigumu mtu kuvumilia katika mazingira aliyokutana nayo siku ya mchezo huo kutokana na kuichachafya ngome ya Yanga na kumdhibi kihuni.
"Baada ya kuonekana tishio kwao waliamua kutumia 'uhuni' kunidhibiti na kwa kuwa refa alikuwa upande wao, walifanikiwa kunitoa mchezoni na kulimwa kadi hiyo ambayo ni ya kwanza kwangu tangu nianze kucheza soka," alisema Juma.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa AFC Arusha, Kagera Sugar na Simba alilimwa kadi hiyo nyekundu na mwamuzi Jacob dakika ya 53 baada ya kumchezea rafu mbaya, Yondani, kabla ya hapo ndiye mchezaji aliyekuwa tishio kwa Yanga.

Mwisho

No comments:

Post a Comment