STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Breaking News: Goli la Kavumbagu laua shabiki Taifa

KAVUMBAGU (KULIA) AKISHANGILIA NA WENZAKE BAADA YA KUIFUNGIA YANGA BAO DHIDI YA AZAM FC KWENYE UWANJA WA TAIFA, DAR, LEO.
Shabiki anayeaminika ni wa Azam FC, ameanguka na baadaye kupoteza maisha, dakika chache baada ya mshambuliaji wa Yanga,  Didier Kavumbagu kuifungia timu yake bao.


Baada ya Kavumbagu kufunga bao hilo, shabiki huyo aliyekuwa amevaa jezi nyeupe na kutambulishwa kwa jina la Deodatus Isaya Mwakiangula.
Imeelezwa Mwakiangula ni meneja wa baa ya Rose iliyo katika eneo la Kimara jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa madaktari viongozi waliokuwa kwenye Uwanja wa Taifa, leo na kumhudumia Mwakiangula kabla ya kupoteza maisha, Nassor Matuzya alithibitisha kuhusu kifo hicho.
Madaktari hao walifanya juhudi kuokoa maisha ya MWakiangula lakini hata hivyo ilishindikana.

Kavumbagu alifunga bao lake katika dakika ya 14, hata hivyo baadaye Azam FC walisawazisha zikiwa zimebaki dakika 8 mpira kwisha kupitia Kelvin Friday.

SALEHJEMBE

No comments:

Post a Comment