STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Yanga, Azam ni vita tupu taifa

Azam Fc

Yanga SC
VITA tupu na pambano la kisasi baina ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga na vinara wa sas wa ligi hiyo, Azam wakati wababe hao wawili watakaposhuka dimbani leo kupepetana katika pambano pekee litakalochezwa uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Yanga itashuka dimbani leo ikiwa na kumbukumbu ya kipigo cha mabao 3-2 iliyopewa na wapinzani wao ambap hawajapoteza mchezo wowote mpaka sasa katika ligi ya msimu huu ikiweka rekodi tangu walipopanda Ligi Kuu msimu wa 2008.
Azam inayoongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 43 itaikabili Yanga ikiwa na kumbukumbu ya ushindo mnono iliyopata kwa mabingwa wa zamani wa kandanda Coastal Union waliowacharaza mabao 4-0, huku Yanga ikishuka Taifa ikitoka kulazimishwa suluhu na mabingwa wa 1990-2000 na 2000-2001,  Mtibwa.
Watetezi wanahitaji ushindi katika mechi hiyo ili kulipa kisasi na pia kupunguza pengo la pointi na wapinzani wao waliowazidi pointi nn4, kwani wenyewe wana pointi 39 licha ya kuwa na mchezo mmoja mkononi.
Hata hivyo mechi hiyo ni ngumu kutabirika kutokana na ubora wa klabu zote mbili ambazo zitawakosa baadhgi ya nyota wao walio majeruhi.
Yanga wenyewe wataikabili Azam ikiwa imekamilika baada ya kurejea dimbani kwa nyota wake kama Haruna Niyonzima, Mrissoh Ngassa na Mbuyi Twitte, licha ya kukosa huduma za kipa Deo Munishi 'Dida;.
Makocha wa timu zote mbili wamenukuliwa kuwa vijana wao wapo tayari kwaajili ya pambano hilo, huku viongozi wa Azam wakiwa na imani kubwa ya kuibuka wababe kwa Yanga ili kutimiza lengo lao la kuwa mabingwa wapya wa Tanzania Bara baada ya kukwama misimu miwili mfululizo wakishika nafasi ya pili.
Je ni Yanga watakaoibuka kidedea na kulipa kisasi katika mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Hashim Abdallah au ni Azam itakayoendelezaubabe na kuking'ang'ania kiti cha uongozi wa ligi hiyo leo? Tusubiri

No comments:

Post a Comment