STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Yanga yabanwa Taifa, Azam yaendeleza rekodi

* Hamis Kiiza 'Diego' akosa penati
Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao lililofungwa na Didier Kavumbagu (wa pili kulia), wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara ilipopambana na Azam  FC kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Timu hizo zilitoka sare ya 1-1. (Picha na Francis Dande)
Heka heka: Golikipa wa timu ya Azam FC, Aishi Salum akiokoa moja ya hatari langoni mwake.
Mfungaji wa bao la Yanga, Didier Kavumbagu akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa Azam FC.
Beki wa Azam FC, Gadiel Michael akimiliki mpira (kushoto) akiwania mpira huo ni mshambuliaji wa yanga, Hamis Kiiza. 
Mashabiki wa Yanga, wakiwa hawaamini timu yao ikibanwa na Azam
Mshambuliaji wa Yanga, simon Msuva akimtoka beki wa Azam FC, Kipre Bolou

BAO la dakika ya 83 lililofungwa na kinda Kelvin Friday lilizima ndoto za Yanga za kutaka kuvunja rekodi ya Azam ya kutopoteza mchezo wowote katika Ligi Kuu Tanzania Bara na kuisaidia vinara hao kupata sare ya bao 1-1 dhidi na watetezi hao.
Yanga waliokuwa wakitaka kulipa kisasi cha kulazwa mabao 3-2 katika mechi ya kwanza bao la uishindi likifungwa pia na kinda mwingine wa Azam, Joseph Kimwaga, watajilaumu baada ya kupata penati iliyopotezwa na mshambuliaji Hamis Kiiza 'Diego'.
Kipa Aishi Manula aliyekuwa nyota wa mchezo huo kwa leo alipangua mkwaju wa Diego na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda kabla ya beki wake wa pembeni, Erasto Nyoni kulimwa kadi baada ya kuzozana na mwamuzi Hashim Abdallah.
Bao la Yanga lililowapa matumaini ya kupunguza pengo la pointi baina yao na vinara hao wa ligi hiyo, liliwekwa kimiani dakika ya 14 kupitia kwa Didier Kavumbagu bao lililodumu hadi mapumziko.
Washambuliaji wa Yanga watajuta kwa kuikosesha mabao timu yao baada ya kukosa mabao mengi ya wazi wakiongozwa na Kiiza, Emmanuel Okwi na Kavumbagu kabla ya Husseni Javu kuingia.
Kwa matokeo hayo ya leo, Azam wameendelea kujiimarisha kileleni kwa kufikisha pointi 44, nne zaidi ya Yanga inayokamata nafasi ya pili ikiwa na pointi 40 na kufuatiwa na Mbeya City yenye pointi 39.
Hata hivyo Yanga bado ina mchezo mmoja mkononi baada ya klucheza mechi 19 wakati Azam imecheza 20.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea wikiendi kwa michezo kadhaa ambapo Yanga itasafiri hadi Tabora kuvaana na Rhino Rangers na Simba itaumana na Coastal Union Mkwakwani Tanga.

No comments:

Post a Comment