STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Askari kanzu, Camera maalum kulinda pambano la Kaseba, Mashali PTA

Kaseba

Mashali
ASKARI kanzu na Kamera Maalum ndizo zitakazotumika kudhibiti hali ya ulinzi katika pambano la kimataifa la ngumi za kulipwa kuwania mkanda wa UBO Afrika kati ya Japeph Kaseba 'Champion' na Thomas Mashali 'Simba Asiyefugika' litakalofanyika Machi 29.
Pambano hilo la uzani wa kati litafanyika kwenye ukumbi wa PTA-Sabasaba jijini Dar es Salaam ambapo kutokana na mabondia hao wawili kuwa na mashabiki wengi, waratibu wake wamepanga kuimarisha ulinzi ili kuwafanya mashabiki watakaofika ukumbini kutokuwa na hofu juu ya usalama wao.
Akizungumza na MICHARAZO, promota wa pambano hilo litakalosindikizwa na michezo mingine kadha ya utangulizi, Ally Mwazoa alisema ili kulinda usalama siku ya mchezo huo watatumia kamera maalum kunasa matukio ndani na nje ya ukumbi ili ikitokea tatizo iwe rahisi kuwabaini wahusika.
Pia alisema mbali na kamera hizo, pia watatumika askari kanzu ambao watakuwa wakifuatilia matukio ndani na nje ya ukumbi ili kuweza kudhibiti uvunjifu wowote wa amani kwenye pambano hilo linalowakutanisha kwa mara ya kwanza Kaseba na Mashali.
Mwazoa alisema utaratibu huo pia utatumika katika pambano litakalofanyika April 26 ambaloo pia ameiandaa yeye kati ya Francis Miyeyusho dhidi ya mtoto wa bingwa wa zamani wa dunia wa WBU, Rashid Matumla, Mohammed Matumla 'Snake Boy Jr'.
Kuhusu maandali ya pambano la Kaseba na Mashali, Mwazoa alisema kila kitu kimekaa vyema na kwamba michezoi ya utangulizi siku hiyo itakuwa ni katika ya Haji Juma dhidi ya Juma Fundi, wakati Fred Sayuni atapambana na Rajabu Mahoja na Zuber Kitandula atamenyana na Issa Omar wakati Bakari Dunda ataoneshana ubabe na Baina Mazola
Pambano jingine lililokuwa liwakutanishe Allen Kamote wa Tanga dhidi ya Fadhil Awadh la kuwania ubingwa wa UBO-Mabara limefutwa kutokana na kifo cha Awadh aliyefariki jijini Dar es Salam baada ya kuugua ghafla na kuzikwa juzi mjini Morogoro.

No comments:

Post a Comment