STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Baby Madaha aachia mbili akiwa Kenya

 



MICHARAZO MITUPU
Baby Madaha katika pozi tofauti
NYOTA wa filamu na muziki nchini anayefanya shughuli zake kwa sasa nchini Kenya, Baby Madaha, ameachia kazi mpya mbili akiwa nchini humo.
Kazi hizo mbili moja ni ya filamu na nyingine ya muziki, fani iliyomtambulisha baada ya kushiriki shindano la kusaka vipaji vya kuimba la BSS.
Akizungumza na MICHARAZO, nyota huyo wa 'single' ya 'Summer Holiday', alisema filamu aliyoiachia inafahamika kwa jina la 'Gell Bladder' aliyoigiza na wasanii kadhaa nyota wa hapa Tanzania akiwamo Mariam Mndeme 'Mamushka' na wengine kutoka Kenya.
Baby alisema kwa upande wa muziki, ameachia 'single' iitwayo 'Mr DJ' ambayo ameirekodia katika studio za Candy Records zinazomilikiwa na 'mabosi' wake anaofanya nao kazi kwa sasa.
"Nimeachia kazi mbili moja ya muziki na nyingine ya filamu. Wimbo unaitwa 'Mr DJ' nimerekodi katika studio za Candy na filamu nimecheza na wasanii kadhaa maarufu wa Kenya na nyumbani yupo Mamushka na mimi mwenyewe," alisema.
Baby Madaha aliyewahi kufunika na wimbo wake wa 'Amore' uliokuja kuzaa albamu yenye jina kama hilo, alisema pamoja na kuachia kazi hizo yupo mbioni kuendelea kuwapa burudani mashabiki wake

No comments:

Post a Comment