STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Chelsea hiyoo robo fainali, Real yaua tena Wajerumani


Etoo akifunga bao la kwanza la Chelsea
Bale akimpongeza Ronaldo baada ya kutupia mpira kambani kutokana na pasi yake
VINARA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea imedhihirisha kiu yao ya kutwaa taji la Liugi ya Mabingwa Ualaya kwa mara nyingine baada ya usiku wa jana kuikwangua Galatasaray ya Uturuki kwa mabao 2-0 na kutinga Robo Fainali.
Mabao ya Samuel Eto'o katika dakika ya nne na jingine la Gary Cahil kwenye dakika ya 43 yalitosha kuivusha vijana na Jose Mourinho na kuwafuta machozi mashabiki wa England ambao wiki iliyopita walishuhudia timu zao mbili za Arsenal na Manchester City ziking'olewa mashindanoni.
Kwa ushindi huo wa jana, Chelsea imeweza kuitupa nje timu ya nyota wa zamani Didier Drogba kwa jumla ya mabao 3-1 kwani katika mchezo wa kwanza walifungana bao 1-1 nchini Uturuki.
Katika mechi nyingine ya michuano hiyo, Real Madrid waliendeleza moto wao kwa kuizabua Schalke 04 ya Ujerumani kwa mabao 3-1 na kusonga robo fainali kwa jumla ya mabao 9-2.
Madrid ikiwa uwanja wa nyumbani wa Santiago Bernabeu ilipata mabao yake kupitia kwa nyota wake ambaye amezidi kuweka rekodi ya mabao kati ligi hiyo Cristiano Ronaldo katika dakika ya 21 na 74 na jingine likifungwa na Alvaro Morata.
Bao la kujifutia machozi la wageni lilitupiwa kambani na Tim Hoogland dakika ya 31 na kuwafanya Schalke kuaga kwa aibu michuano hiyo kwa msimu huu.
Katika mfululizo wa mechi za ligi hiyo kumaliza timu za mwisho za kutinga robo fainali, Manchester United itakuwa nyumbani kuikaribisha Olympiacos ya Ugiriki waliowatambia kwao kwa mabao 2-0  nayo timu ya Borussia Dotmund itaikaribisha Zenit.  Katika mechi yao ya kwanza Wajerumani walishinda ugenini kwa 4-2
Timu sita za kwanza kufuzu robo fainali ya michuano hiyo kwa mwaka huu ni watetezi Bayern Munich, Barcelona, Atletico Madrid, PSG, Chelsea na Real Madrid

No comments:

Post a Comment