STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 19, 2014

Dar Modern kuuza sura videoni


KUNDI la Dar Modern 'Wana wa Jiji' lipo wilayani Lushoto-Tanga likirekodia video za nyimbo za albam zao mbili walizozizindua hivi karibuni wakati wakiwatambulisha wasanii wao wapya.
Akizungumza na MICHARAZO kutoka Lushoto, mmoja wa waimbaji nyota wa kundi hilo, Hassan Kumbi 'Hassani Vocha', alisema tayari asilimia kubwa ya video hizo zimesharekodiwa.
Albamu hizo ni; 'Oh My Honey' na 'Kitwitwi' zenye nyimbo kama 'Oh My Honey', 'Naenda kwa Mume Wangu', 'Sikuamini Macho Yangu' na 'Malipo Duniani', 'Kitwitwi', 'Ngoma Imepasuka' na 'Siwanyimi Uzuri'.
Dar Modern ilianzishwa mwaka 2006 na imeshatoa albamu zaidi ya tano zikiwamo za 'Ni Vijimambo Tu', 'Sote Twasaka Riziki', 'Gharika la Moyo (Pembe la Ng'ombe)', 'Ndugu wa Mume Mna Hila', 'Toto la Kiafrika' na 'Nauvua Ushoga'.

No comments:

Post a Comment