STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 2, 2014

Kipusa cha Kaole Sanaa chatambulishwa kwa wadau

Sehemu ya igizo hilo kama lilivyokuwa likionekana kwenye screen
Wadau wakipata uhondo wa Kipusa
Iizo likiendelea kwenye runinga
Wadau na wasanii walioshiriki igizo hilo wakifuatilia kwa makini
Joti aliyekuwa Mwenyekiti wa Muda wa kujadili igizo hilo akizuingumza na wadau waliohudhuria onyesho hilo
We kichwa bana na mkikomaa mtafika mbali na kuleta mapinduzi katika tasnia yetu: Ni kama Raia wa TAFF Simon Mwakifamba akimwambia Katibu wa New Kaole Sanaa, Issa Kipemba
Rais wa TAFF, Simon Mwakifanya (kulia) akitoa nasaha zake huku Joti akimsikiliza kwa makini
Simon Mwakifamba Rais wa TAFF akiwa na Mwenyekiti wa New Kaole, Ndimbangwe Misayo 'Thea'.
Mabrekaaaa! Swebe Santana (kulia) Bi Staa na Bi Terry nao walikuwapo na Muongozaji wa filamu hiyo, Christant Mhengga akionekana kwa nyuma yao (shati jeusi)

Yaani ilikuwa ni fursa ya kuwaona wasanii wakali waliosahaulika kitambo
Nyie wenyewe mmeiona ni bab' kubwa---Joti akizungumza leo
Wadau wakiwa makini kufuatilia igizo kwenye runinga
Ilikuwa ni full burudani toka kwa wakali hao waliokumbusha enzi zao kupitia KIPUSA
Watu walikuwa makini kufuatilia
Chifu Husseni Msopa, Sheikh Sadik Godegode na Sheikh Kassim wakiwa makini kufuatilia igizo hilo
Abdallah Mkumbira 'Muhogo Mchungu' Makamu Mwenyekiti wa New Kaole na mmoja walioling'arisha igizo hilo la Kipusa naye alikuwapo kujishuhudia.
Oyaa umeona pale da! Kama wanaambizana Chifu Msopa na Sheikh Godegode
Watu walikuwa makini kupita maelezo
Viongozi wa Kaole, waigizaji wa Kipusa na wageni mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya hafla hiyo
 

Hakuna aliyetaka kupitwa na uhondo
Sehemu ya waliohudhuria wakiwa katika picha ya pamoja na wasanii walioshiriki igizo la Kipusa
Muongozaji mahiri wa tamthilia na filamu nchini, Christant Mhengga akitoa nasaha zake
Mwenyekiti wa Kaole Sanaa, Ndimbangwe Misayo 'Thea' akizungumza yake kushukuru wadau waliohudhuria
Kusudio letu ni hili....Thea akizungumza
Kama Mwinjilisti! Thea akiendesha dua maalum ya kufungia hafla mbele ya wadau

'Tunakuomba kwa Jina la Bwana Yesu Kristo Ameen" Wadau wakiwa makini wakati dua maalum iliyoendeshwa na Thea
KUNDI la Kaole Sanaa ambalo kwa karibu miaka 10 lilikuwa kimya, leo limeitambulisha kwa wadau wao tamthilia yao mpya iitwayo 'Kipusa' inayowarejesha rasmi katika ulimwengu wa sanaa nchini.

Utambulisho wa tamthilia hiyo inayorejesha kumbukumbu ya enzi za kundi hilo lilipokuwa likitisika anga la sanaa, ulifanyika kwenye ukumbi wa Dar Modern, uliopo Magomeni Mikumi, jijini Dar es Salaam.
Pamoja na kuwaonjesha kidogo uhondo mzima wa tamthilia hiyo, lakini wadau waliohudhuria waliburudika vya kutosha na kuwasifia wasanii walioanzisha wazo hilo la kurejesha kundi hilo.
Baadhi ya wadau waliopata nafasi ya kutoa maoni yao baada ya kushuhudia sehemu mbili kati ya 25 za tamthilia hiyo walikiri Kaole ni Baba wa Sanaa na kuwataka wasanii hao kutorudi nyuma.
Miongoni mwa waliohudhuria ni Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifamba, viongozi wa Taasisi ya Amani Tanzania, Sheikh Sadik Godegode na Mwenyekiti wa Baraza la Habari la Kiislam (BAHAKITA), Chifu Hussen Msopa.
Katika nasaha zake ndogo Rais wa TAFF aliwasifia viongozi na wasanii wa Kaole kwa kutoa wazo la kulirejesha kundi hilo na kudai kuwa wao ndiyo wasanii wa ukweli na wanaojua wanachokifanya.
Mwakifamba pia aliwasisitizia kundi hilo kulenga soko la kimataifa ili angalau Tanzania iweze kutamba na kunyakua tuzo kama ambavyo wasanii wa mataifa ya Nigeria, Kenya na nchi nyingine.
Mwenyekiti wa kundi hilo, Ndimbangwe Misayo 'Thea' aliwashukuru waliohudhuria na kuwataka waendelee kuwaunga mkono katika safari yao ambayo ndiyo kwanza wameianza.
Naye Muongozaji na mmoja wa waasisi wa kundi hilo, Christant Mhenga, alisema anachukua maoni, ushauri na hata ukosoaji uliotolewa na baadhi ya wadau kama changamoto za kuboresha kazi yao.
Msanii wa muziki, Vitalis Maembe 'Mzee wa Sumu ya Teja' aliahidi kuwapiga tafu Kaole ili kuendeleza mipango yao ya kurejesha heshima ya sanaa ya maigizo nchini.

No comments:

Post a Comment