STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 6, 2014

Malaga yachinja mtu 4 nyumbani

http://www.bettingtipository.com/wp-content/uploads/2013/04/granada_vs_malaga_121209a-480x330.jpg
MABAO mawili yaliyofungwa na Ignacio Camacho yaliisaidia Malaga kupata ushindi mnono wa mabao 4-1 nyumbani dhidi ya Grenada katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Hispania.
Mfungaji huyo alifunga mabao yake katika dakika ya 14 na 37 na mengine mawili toka kwa Amrabat  kwa mkwaju wa penati na Juanmi yaliiwezesha Malaga kuzoa pointi tatu.
Amrabat alifungwa katika dakika ya 50 na lile la Juanmi lilifungwa kwenyue dakika ya 74 na kuwapa uongozi wenyeji wa mabao 4-0 kabla ya wageni kuchomoa bao moja dakika ya 78 lililofungwa na Yousef El Arabi.
Malaga imepanda hadi nafasi ya 11kwa kufikisha pointi 38 ikiipita Celta Vigo na wapinzani wao wameporomoka hadi nafasi ya 14 ikisaliwa na pointi zake 34.
Ligi hiyo baod inaongozwa na Atletico Madrid yenye pointiu 79 na kufuatiwa na Barcelona yenye pointi 78 kisha Real Madrid iliyokusanya pointi 76.

No comments:

Post a Comment