STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 6, 2014

Lazio, Fiorentina, Roma zashinda Italia

http://e1.365dm.com/14/01/768x432/Lazio-Celeb-v-Inter_3062528.jpg?20140106200749
Lazio
http://hasilprediksibola.com/wp-content/uploads/2013/12/Prediksi-Sassuolo-vs-Fiorentina.jpg
Fiorentina
 KLABU za Lazio, Fiorentina na Roma zimezidi kujiimarisha katika nafasi zao za Ligi Kuu ya Serie A baada ya kupata ushindi katika mechi za ligi hiyo zilizochezwa leo.
Lazio wakiwa nyumbani na ikicheza pungufu ya mchezaji wake Biglia kuonyesha kadi ya pili ya njano na kufuatiwa nyekundu dakika ya 57, waliifumua Sampdoria kwa mabao 2-0 , yaliyotupia kambani na Candreva katika dakika 42 na Lulic kwenye dakika ya 73.
Roma wakiwa ugenini waliifumua bila huruma Cagliari kwa mabao 3-1, huku Sassuolo ikipata ushindi pia ugenini wa mabao 2-0 dhidi ya Atalanta na Catania ikafa nyumbani kwao mbele ya Torino, wakati Fiorentina iliishinda 2-1 dhidi ya wageni wao Udinese.
Baadaye usiku Parma watapepetana na Napoli katika 'bonge' la mechi linalosubiriwa kwa hamu kabla ya Jumatatu kushuhudiwa mitanange mingine ya ligi hiyo kwa watetezi Juventuskuikaribisha Lirvono na AC Milan kuwafuata Genoa.

No comments:

Post a Comment