STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 6, 2014

Arsenal yasulubiwa na Everton x3

Romelu Lukaku
Romelu Lukaku akishangilia bao walipokuwa wakiisulubu Arsenal muda mfupi uliopita
NDOTO za klabu ya Arsenal kuweza kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya England, imezidi kufifia baada ya mapema leo kudunguliwa mabao 3-0 na Everton.
Mabao ya Steven Naismith katika dakika ya 14 na jingine la Romelu Lukaku katika dakika ya 34 yalitosha kuwpaa uongozi wenyeji wa mabao 2-0 hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kulikuwa na kosa kosa za hapa na pale mpaka pale Mikel Arteta alipojifunga bao katika dakika ya 62 katrika harakati za kuokoa bao langoni mwake.
Kwea ushindi huo Everton imejiimarisha kwenye nafasi ya tano ikifikisha pointi 63 moja zaidi ya Arsenal waliosalia kwenye nafasi ya nne wakati ligi ikielekea ukingoni.
Ligi hiyo itaendelea tena muda mfupi ujao kwa Liverpool kuwa wageni wa West Ham United kabla ya kesho Tottenham Hotspur kuialika Sunderland kwenye uwanja wao wa White Hart Lane.

No comments:

Post a Comment